Akpan Mambo Magumu Simba, Kocha Zoran Amkataa Live

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KIUNGO wa Simba, Victor Akpan huenda akatolewa kwa mkopo kutokana na kushindwa kumshawishi kocha, Zoran Maki ili kumpatia nafasi ya kucheza katika michezo mitatu iliyocheza timu hiyo hadi sasa.

Akpan alisajiliwa na Simba kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Coastal Union baada ya kuonyesha kiwango bora msimu uliopita kwenye Ligi Kuu Bara pamoja na kombe la Shirikisho (ASFC).

Akpan anacheza nafasi ya kiungo mkabaji ambayo kwenye mechi dhidi ya St George, Yanga na Geita Gold walitumika, Jonas Mkude, Sadio Kanoute na Mzamiru Yassin ambao wawili hawa hawakuwa kwenye pre-season kule Misri.

Inaelezwa kutokana na Akpan kushindwa kumshawishi, Zoran huenda akarudishwa kwa mkopo Coastal Union na nafasi yake ikachukuliwa na kiungo mpya kutokea Kwara United FC kutokea Ligi Kuu ya Nigeria, Afeez Nosiru.


Mabosi wa Simba inaelezwa wameanza mchakato wa kutafuta kiungo mpya wa ukabaji na Nosiru anapewa nafasi kama chaguo la kwanza ingawa kuna chaguo la pili kama kiungo wa zamani wa Kaizer Chiefs, Teddy Akumu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad