Karani wa Sensa Aporwa Kishikwambi Cha Kuhesabia Sensa, Mme Akijeruhiwa Arusha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Karani aporwa kishikwambi
KARANI wa Sensa ya Watu na Makazi Jiji la Arusha, Sarapia Kiwango ameporwa kishikwambi chake wakati akijiandaa kwenda kuhesabu makundi maalum jana usiku huku mume wake akijeruhiwa.

Akizungumza na mwandishi wa HabariLEO, Mratibu wa sensa ya watu na makazi katika Jiji la Arusha, Maneno Maziku amesema Kiwango aliporwa kishikwambi usiku wakati akienda kuhesabu makundi maalum huku mume wake akijeruhiwa kichwani.

Amesema baada ya tukio hilo Karani huyo alipewa kishikwambi kingine na anaendelea na kazi.

“Ni kweli aliporwa kishikwambi na mume wake kujeruhiwa kichwani lakini ameshapewa kishikwambi kingine anaendelea na kazi lakini pia majeruhi hali yake inaendelea vizuri,” amesema Maziku.

Diwani wa Kata ya Unga Limited, Mahamod Said na Mtendaji wa Kata hiyo, Sophia Laizer wamesema karani huyo alivamiwa na watu waliokuwa na boda boda na kumpora kishikwambi hicho.

“Jana usiku hawa makarani wa sensa waliitwa kwa mtendaji, wakati wanakwenda huko ndiyo akakutana na vibaka waliokuwa kwenye bodaboda wakamjeruhi mumewe na kumpora kishikwambi kisha kutoweka kusikojilikana,” amefafanua Said.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad