AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
MWANARIADHA wa Tanzania wa mbio fupi kwa wanawake, Winfrida Makenji ameondolewa kushiriki mashindano ya mbio fupi yanayoendelea jijini Birmingham, Uingereza.
Winfrida ameondolewa kwenye michuano hiyo leo Agosti 2, 2022 baada ya kukutwa na kosa katika kuanza mbio za mita 100 katika Uwanja wa michezo wa Alexander jijini Birmingham, Uingereza.
Katika taarifa ya Kocha wa Raidha, Suleiman Nyambui iliyotumwa kwenye vyombo vya Habari, inasema kuwa hofu, kukosa uzoefu vimechangiwa kwa mchezaji huyo kuondolewa mashindanoni.
“Winfrida ni mkimbiaji hodari ila hofu ya mashindano pamoja na kukosa uzoefu wa kushindana mara kwa mara vimechangia kuondolewa kwake mwanzo tu wa kuanza mbio.” Amesema Nyambui
Amesema Winfrida alifanya kosa la kuchomoka kabla ya mlio wa bastola ya kuanzia kulia, ambapo katika mashindano makubwa kama hayo adhabu yake ni kutolewa (disqualified).
Hata hivyo, Nyambui amesema kuwa Winfrida bado ana nafasi ya kushiriki mchuano wa mbio za mita 200 ambao atashindana siku ya Alhamisi Agosti 4, 2022, ambapo atakimbia raundi ya kwanza. Akipita ataingia raundi ya pili siku ya pili Agosti 5.
Aidha, Nyambui amesema kesho kutwa Alhamisi Agosti 4 mwanariadha Andrew Boniface Rhobi ataingia uwanjani kuchuana katika mbio za mita 1,500.
Rhobi, ambaye ana umri wa miaka 32 atajiunga na wanariadha wengine wa nchi mbalimbali kujaribu kuvunja rekodi ya mbio hizo za mita 1500 inayoshikiliwa na Mtanzania mwingine Filbert Bayi kwa miaka
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK