Ni Hukumu ya Kuitikisa Katiba au Wanasiasa Kenya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Nairobi. Tofauti na hukumu iliyofuta ushindi wa Uhuru Kenyatta mwaka 2017, ya leo inaweza kutikisa Katiba ya Kenya kutokana na hoja za walalamikaji ambao ni Raila Odinga na Martha Karua.

Mbali na hayo, makamishna wanne kati ya saba wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) walijitenga na matokeo yaliyotangazwa hivyo kuongeza ugumu kama wataweza kuungana iwapo matokeo ya urais yaliyotangazwa yatafutwa.

Hukumu hiyo inatolewa baada ya Odinga aliyekuwa mgombea urais kupitia muungano wa Azimio la Umoja-One Kenya na mgombea mwenza wake, Martha Karua kupinga katika Mahakama ya Juu ushindi wa mgombea wa muungano wa UDA, Dk William Ruto.

Wawili hao mbali na kuiomba mahakama iwatangaze wao kuwa washindi wa uchaguzi huo uliofanyika Agosti 9, wameomba IEBC itangazwe kutokuwa na uwezo wa kusimamia uchaguzi na kumtangaza mwenyekiti wake, Wafula Chebukati kukosa sifa za kuongoza ofisi hiyo ya umma.


Tayari Jaji Mkuu Martha Koome na msaidizi wake Philomena Mwilu, wamewaomba Wakenya wawaombee ili leo watoe uamuzi wenye busara na unaoendeleza demokrasia nchini humo.

Majaji wengine kwenye kesi hiyo ni Mohamed Ibrahim, Dk Smokin Wanjala, Njoki Susanna Ndung’u, Isaac Lenaola na William Ouko.

Wakati wa uamuzi wa kupinga ushindi wa Uhuru Kenyatta mwaka 2017 katika kesi iliyofunguliwa na Raila Odinga, Jaji Mkuu David Maranga alisema kati ya majaji sita waliosikiliza kesi hiyo wanne walijiridhisha kwamba uchaguzi huo haukufanyika kwa mujibu wa Katiba na sheria za uchaguzi nchini humo.


Hukumu ya leo ina majaji saba wakiongozwa na Martha Koome aliyezaliwa mwaka 1960 ambaye ni jaji mkuu wa 15 tangu Kenya ipate uhuru.

Wakati akifuta ushindi wa Uhuru Kenyatta, Jaji Mkuu Maranga alisema kwa mujibu wa majaji hao kulikuwa na udanganyifu mkubwa kwenye uchaguzi huo hivyo haukuwa huru wala kufanyika kwa haki.

Kauli ya Jaji Maranga iliungwa mkono na Chekubati ambaye baada ya hukumu hiyo alinukuliwa akisema waliohusika katika kuvuruga uchaguzi wanafaa kuwajibishwa.

Pia, alitangaza kumwalika Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) kufanya uchunguzi ndani ya IEBC na kuwafungulia mashtaka watu wote waliohusika kuuvuruga uchaguzi.


Tangu hukumu hiyo ya Agosti 2017, Odinga ameendelea kuilalamikia IEBC na katika maombi yake kwenye kesi inayotolewa hukumu leo ni kwamba imeshindwa kusimamia uchaguzi na Chekubati hana uwezo wa kuongoza ofisi hiyo ya umma.

Mgongano wa kikatiba

Iwapo leo Mahakama ya Juu itaufuta ushindi wa Dk Ruto, kwa mujibu wa Katiba uchaguzi huo mkuu utatakiwa kurudiwa ndani ya siku 60.

Pia, kama mahakama itakubaliana na hoja za Odinga za kuitangaza IEBC kutokuwa na uwezo wa kusimamia uchaguzi au mwenyekiti wake Chekubati kwamba hana uwezo wa kuiongoza ofisi hiyo ya umma, Kenya itaingia kwenye mgogoro wa kikatiba kwa kuwa Rais Uhuru Kenyatta anayeondoka madarakani hana madaraka ya kuteuwa kiongozi yeyote, anachosubiri ni kuapishwa kwa Rais mpya yeye aondoke.

Hata hivyo, Katiba inaelekeza kuwa kiongozi wa IEBC anaweza kuondolewa kwa mashitaka dhidi yake kuwasilishwa bungeni na tume maalumu itakayoundwa na Rais.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad