AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jeshi la Polisi mkoa wa Mara limesema kwamba Askari wake wamekuwa wakitenda majukumu yao kwa weledi na kwamba tukio la msichana kutendewa isivyo kwa kuvuliwa nguo ni la kutengenezwa halina ukweli wowote.
Taarifa hiyo imetolewa hivi karibuni na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara ACP Longinus Tibishubwamu, kupitia mkutano ulioandaliwa kwa njia ya mtandao.
"Askari wetu wanafanya kazi kwa weledi na watu wanaotupiga vita hilo tukio (tuhuma za binti kutotendewa isivyo stahili) wamelipika hicho kitu hakipo, hilo limepikwa ili kuchafua kazi nzuri ya jeshi la polisi, hivyo taarifa ya msichana sijui kuvuliwa nguo ni potofu na kwa ujumla mkoa wa Mara ni shwari," amesema Kamanda Tibishubwamu
"Taarifa za upotoshaji kuhusu utendaji wetu wa kazi naomba wananchi wazipuuze na wale wanaotoa taarifa zile wapuuzwe kwa sababu ni ajabu mtu mwenye akili timamu kutetea jambazi linaloua na kupora watu kwa bunduki ya kivita," ameongeza Kamanda Tibishubwamu
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK