Philip Mpango "Viongozi Jiepusheni na Walinzi na Waandishi Binafsi Kwa Usalama Wenu na Kuvuja Siri za Serikali"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango amefungua Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Wilaya Tanzania Bara Jijini Dodoma leo ambapo amewataka Viongozi kujiepusha na matumizi ya Walinzi binafsi na Waandishi wa Habari binafsi bila kufuata taratibu kwakuwa inahatarisha usalama wao binafsi na wa siri za Serikali.

“Naamini Watoa mada mtatoa msisitizo kuhusu matumizi ya Walinzi binafsi, wamekuwepo Watu wanajichukulia Walinzi binafsi (Body Guard) na Waandishi wa Habari binafsi katika Ofisi za Umma, sasa zipo taratibu za kufuata endapo itabainika Kiongozi anahitaji kupatiwa Wasaidizi wa aina hii kwahiyo zingatieni taratibu zilizopo na sio vinginevyo”

“Kiongozi asipofuata utaratibu unaotakiwa kuwapata Watumishi hawa na kuamua kujitafutia mwenyewe wakati mwingine inakuwa sio salama hata kwa Kiongozi mwenyewe na hata siri za Serikali”

“Kuweni makini na maneno mnayozungumza kupigapiga story na Wasaidizi wenu hususani Madereva wetu na Watu wengine mnapokuwa nje ya Ofisi zenu au hata sehemu za starehe ili kuepuka kutoa siri za Serikali”
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad