Kumekucha..Kenya Yakiri Wazi Wazi Kukumbwa na Ukata wa Fedha, Wafanya Kazi Kugoma

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Serikali ya Kenya imekiri kwamba inakabiliwa na uhaba wa pesa ambao umechelewesha malipo ya mishahara ya maelfu ya wafanyikazi wa umma.

Inasema ilibidi kufanya maamuzi magumu iwapo italipa mishahara au kulipa mamilioni ya dola katika deni la nje, linalodaiwa mwezi huu.

Hazina ya kitaifa pia imeshindwa kutuma pesa kwa serikali za kaunti - vitengo vilivyogatuliwa ambavyo vinasimamia huduma za umma kama vile afya na elimu.

Wafanyikazi katika wizara, mashirika na serikali za kaunti ndio wameathiriwa zaidi na ucheleweshaji wa mishahara ya Machi.

Waziri wa Fedha Njuguna Ndung'u alisema serikali inakabiliwa na matatizo ya kifedha yanayosababishwa na mapato adimu na na mzigo wa madeni.

Vyama viwili vinavyowakilisha wafanyikazi wa serikali ya kitaifa na kaunti vimetoa notisi za nia yao ya kususia kazi.

Naibu Rais Rigathi Gachagua amelaumu mzozo huo kwa serikali ya zamani ambayo anaituhumu kwa kukopa pesa nyingi ikiwa mamlakani na kuvamia hazina kabla ya kuondoka mamlakani mwaka jana.Lakini hakutoa ushahidi wowote wa madai hayo.

Mshauri wa rais wa masuala ya uchumi David Ndii alisema mishahara iliyocheleweshwa sio shida na akataja hali kama "Changamoto ya upatikanaji wa hela".

Katika mahojiano ya runinga, Bw Ndii alisema kuwa serikali ilikuwa inatarajia $500m (£460m) kutoka kwa mkopo ulioidhinishwa na mishahara ya watumishi wa umma italipwa mwishoni mwa wiki ijayo.

Deni la umma la Kenya sasa linafikia 65% ya mapato.

Nchi hiyo inahitaji zaidi ya $420m kila mwezi kulipa mishahara na pensheni kwa watumishi wa umma.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad