AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
USM Alger walifanikiwa kutinga fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kuwaondosha Asec Mimosas ya Ivory Coast na wanatarajiwa kukipiga dhidi ya Yanga ambapo wataanzia ugenini kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar Mei 28 na kisha watamalizia kwenye uwanja wao wa nyumbani Juni 3 nchini Algeria.
Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo, kocha Benchikha amesema kuwa anatarajiwa kupata upinzani mkubwa kutokana na kuwa ni mchezo wa fainali na huku akiweka wazi kuwa hakuna timu ambayo imetinga fainali itatamani kupoteza katika mchezo wa Fainali.
“Hakuna timu ambayo imetinga katika hatua ya fainali itatamani kuona kuwa inapoteza mchezo huo, hapo ndio ugumu wa mchezo huanza kuonekana kwa kuwa upinzani huwa ni mkubwa.”
“Hakuna fainali ambayo huwa nyepesi hivyo naamini tunakwenda kukutana na upinzani mkali kutoka kwa wenzetu, tunafahamu kuwa tunatakiwa kushinda lakini haitakuwa rahisi kama watu wanavyoona,” amesema kocha huyo
Miongoni mwa nyota wa Young Africans ambaye amekuwa kwenye kiwango cha juu katika kombe hilo ni Mshambuliaji kutoka DR Congo Fiston Mayele ambaye amefunga mabao sita akiwa na uhakika wa kubeba kiatu cha ufungaji bora wa michuano hiyo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK