Kocha Nasreddine Nabi aishtukia Janja ya USMA , Hawa Lazima Tuwale Kichwa Kwao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kocha Nasreddine Nabi aishtukia Janja ya USMA , Hawa Lazima Tuwale Kichwa Kwao
Kocha Nabi


Kocha wa Young Africans Nasreddine Nabi amesema ameshtukia baadhi ya mambo na anatarajia kubadili mfumo katika Mchezo wa Mkondo wa Pili wa Fainali, Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya USMA.


Baada ya juzi Jumapili (Mei 28) Young Africans kupoteza kwa kuchapwa 2-1, sasa wameanza mikakati ya mchezo wa Mkondo wa Pili utakayopiga Jumamosi (Juni 03) katika Uwanja wa Stade du 5 Juille.


Nabi amesema mchezo wa juzi Jumapili pale Uwanja wa Benjamin Mkapa aligundua ni wapi USM Alger waliwazidi ujanja.


“Yaliyotokea ni matokeo. Tulifanya baadhi ya makosa yaliyotufanya kupoteza mechi lakini bado tuna dakika 90 nyingine ugenini, na kuna mambo tumeshayagundua,” amesema.


“USM Alger ni timu bora na yenye wachezaji wachangamfu. Natambua ugumu wao hususan kwenye mechi ya ugenini lakini naamini tutajipanga upya na kwenda kutafuta matokeo mazuri kwao kwa kuwa tuna uwezo huo.”


Hata hivyo huenda Nabi akabadili mfumo na baadhi ya wachezaji katika kikosi alichokianzisha katika mchezo wa nyumbani Dar es salaam.


Young Africans inahitaji ushindi wa kuanzia mabao 2-0 ugenini ili kutwaa taji na kama itashinda 2-1 kama ilivyofungwa nyumbani basi mchezo utamaamuliwa kwa mikwaju ya Penati.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad