BUNGENI: Waziri Mbalawa "Gharama ya Kupaki Meli Nangani Kwa Siku ni Shilingi Milioni 58"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Waziri wa Ujenzi Prof. Makame Mbarawa leo June 10,2023 amewasilisha Bungeni maelezo ya awali kuhusu mapendekezo ya kuridhia mkataba baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kuhusu ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa ajili ya uendelezaji na uboreshaji wa utendaji kazi wa Bandari Tanzania ambapo amesema kutokana na ufanisi mdogo wa Bandari ya Dar es salaam kwa sasa gharama za meli kusubiri nangani kwa siku moja ni takriban Dola za Marekani 25,000, sawa na takriban Shilingi milioni 58 kwa siku.

“Athari za kutokuwa na ufanisi katika Bandari ya Dar es Salaam ni pamoja na meli kusubiri muda mrefu nangani ambako kunasababisha kuongezeka kwa gharama ya kutumia bandari ya Dar es Salaam, kwa mfano gharama za meli kusubiri nangani kwa siku moja ni takriban Dola za Marekani 25,000, sawa na takriban Shilingi milioni 58 kwa siku, meli kutumia muda mrefu kupakia na kupakua shehena gatini kwa wastani wa siku 5 ikilinganishwa na siku 1 inayokubalika kimataifa, meli kubwa kutokuja katika bandari ya Dar es Salaam kutokana na kuchukua muda mrefu kuhudumiwa”

“Hali hii husababisha bandari yetu kuwa Bandari inayolishwa shehena na Bandari zingine na kuongeza gharama ya kutumia Bandari hiyo na kuikosesha nchi mapato ambayo yangeweza kutumika katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati nchini ambayo ingesaidia kukuza uchumi na kuboresha huduma za Wananchi”

“Pia, kunaongeza gharama katika mnyororo mzima wa usafirishaji kutoka nje ya nchi, kupitia katika Bandari yetu kwenda nchi za jirani zinazotumia Bandari hiyo, kwa mfano, gharama ya kusafirisha kasha moja kutoka nje ya nchi kwenda DRC zinafikia takriban Dola za Marekani kati ya 8,500 hadi 12,000, hii ni gharama kubwa sana ikilinganishwa na Bandari shindani”
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad