Fiston Mayele na Kocha Nabi Kutimkia South Africa Baada ya Kukomba Tuzo Kibabe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Fiston Mayele na Kocha Nabi Kutimkia South Africa Baada ya Kukomba Tuzo Kibabe
Mayele na Kocha Nabi

Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine huenda akaachana na Yanga baada ya msimu huu kuisha.

Bosi huyo wa Young Africans SC alitoa taarifa kwa kikosi chake wikendi hii kabla ya parade la Ubingwa kuwa atawaacha Wananchi mwishoni mwa kandarasi yake.

Baada ya kukataa pendekezo la kuongezewa mkataba wa miaka miwili mipya, kocha huyo wa Tunisia anatafuta changamoto mpya katika maisha yake ya soka baada ya kushinda mataji matatu ya nyumbani msimu huu na kutinga fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF.

Kaizer Chiefs kwa mara ya kwanza waliongea na kocha Nabi takribani wiki mbili zilizopita, na baada mazungumzo ya awali, pande zote mbili zilikubali kuwa wasubiri mchezo wa fainali ya FA upite ndipo waanze kuzungumzia maslahi binafsi.

Awali Nabi alipokea ofa nzuri kutoka kwa Raja Club Athletic, Wydad Athletic Club na Esperance katika miezi ya hivi karibuni lakini akakataa ombi lao la kutaka kuondoka Yanga katika kipindi ambacho ligi zilikua hazijaisha na bado walikuwa wanawania vikombe viwili.

Nabi amewapa masharti Kaizer Chiefs ya kwenda na kocha wake msaidizi, kocha wa makipa, na kocha wa viungo, iwapo atateuliwa kuwa kiongozi wa kuinoa miamba hiyo ya Soweto msimu ujao.

Ikiwa Kaizer Chiefs watakuwa tayari kukubali masharti au kuingia kwenye mazungumzo zaidi, bosi huyo wa zamani wa Al-Merrikh SC anaweza kuwasili mapema wiki ijayo kuhitimisha hatua hiyo lakini kwa jinsi mambo yalivyo, ni kugusa na kwenda.

Kwenye dili hili huenda kocha Nasredine nabi akaondoka na Fiston Mayele ambaye pia Kaizer Chiefs wameonyesha nia ya kumtaka.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad