AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
WANAUME wawili waliokuwa na matatizo ya nguvu za kiume kutokana na matatizo mbali mbali ya kiafya, wamefanyiwa upasuaji na kupandikizwa uume katika Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Bingwa wa upasuaji wa mfumo wa mkojo nchini (TAUS) pamoja na Daktari bingwa kutoka nchini Ufaransa.
Upasuaji huo wa kupandikiza uume umefanyika katika hospitali hiyo iliyopo mkoani Dodoma kwa mara ya kwanza.
Akizungumza Daktari Bingwa wa magonjwa ya mfumo wa mkojo kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa Remigius Rugakingira amesema upandikizaji huo wa uume umefanyika kwa mara ya kwanza nchini.
“Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufanya upasuaji wa aina hii kilichofanyika hapa ni kuweka vipandikizi maalumu vitakavyowezesha uume kurudi katika hali yake ya kufanya kazi.”Amesema
Dkt. Rugakingira amesema Hospitali ya Benjamin Mkapa inajali afya ya Wanaume na upasuaji kama huu unaweza kufanyika Tanzania na kuwataka wanaume wenye matatizo ya nguvu za kiume kufika hospitali ya BMH kufanya upasuaji wa kuweka vipandikizi kwenye uume kwani ndio hospitali pekee kwa sasa inayotoa huduma hiyo hapa nchini.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK