AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro linawashikilia watu watano kwa tuhuma za mauaji ya Khudheifa Changa (26), ambaye alikuwa ni Muuguzi wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC Moshi, Kilimanjaro.
Inadaiwa Khudheifa Changa aliuawa usiku wa kuamkia Julai 2, mwaka huu wakati akipita katika uchochoro wa Mtaa wa Marindi mjini Moshi, katika purukushani alijeruhiwa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali kwenye mbavu ya kushoto usawa wa moyo.
"Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na raia wema lilifanikiwa kupata taarifa zilizosaidia kukamatwa kwa watuhumiwa watano ambao walitoweka baada ya kutenda unyama huo, na watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika," amesema ACP Maigwa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ACP Simon Maigwa, amesema kuwa watuhumiwa hao ambao watatu ni wanaume na wanawake wawili walikuwa na nia ya kumpora mali alizonazo, na kwamba watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.
Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC Gabriel Chisseo amesema marehemu alianza kazi Februari Mosi mwaka huu akiwa amekaa kazini kwa miezi minne hadi umauti ulipomkuta.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK