Mwanafunzi wa Chuo cha Uhasibu (TIA) Ajinyonga Hadi Kufa, Aandika Haya Whats App Status

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanafunzi wa Chuo cha Uhasibu (TIA) Mkoani Mtwara aliyetambulika kwa jina moja la Regan ambaye amekuwa akiishi Mtaa wa Chikongola, Manispaa ya Mtwara- Mikindani anadaiwa kujinyonga hadi kufariki na mwili wake kukutwa ndani ya chumba chake.

Taarifa za kifo chake zilianza kusambaa jana July 4,2023 majira ya saa sita mchana na hadi sasa sababu zilizofanya ajitoe uhai hazijajulikana.

Baadhi ya Mashuhuda wameeleza hisia zao na kusema huenda Kijana huyo aliamua kujitoa uhai kutokana na masuala ya kimapenzi kwasababu Siku sio nyingi alikua amegombana na Mpenzi wake waliyekuwa wakiishi pamoja.

Kamanda wa wa Mtwara Nicodemus Katembo amesema amepokea taarifa za tukio hilo na atalitolea ufafanuzi baada ya uchunguzi wa Madaktari kukamilika na kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Ligula.

Marehemu Reagan muda mfupi kabla ya kujitoa uhai aliweka picha yake ya utoto kwenye WhatsApp Status yake na kuandika maneno yafuatayo ——> “🙏🏾 kwa jasho lako utajipatia chakula mpaka utakaporudi udongoni ulimotwaliwa, maana WEWE NI MAVUMBI NA MAVUMBINI UTARUDI”
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad