Benard Morrison Kuwashtaki Yanga FIFA, Mto Taarifa Afunguka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



TAARIFA ambazo Championi Ijumaa zimepata ni kuhusiana na kiungo raia wa Ghana ambaye amepita Yanga na Simba, Bernard Morrison kutaka kwenda tena Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).

Taarifa kutoka kwa mtu wa karibu kabisa na nyota huyo zimeeleza kuwa Morrison anaweza kwenda tena FIFA kuwashtaki Yanga kama wakishindwa kumpa stahiki zake ambazo anawadai.

Mtoa taarifa huyo alisema, ameambiwa na Morrison kuwa amewapa Yanga muda wa kuhakikisha kuwa analipwa fedha hizo na kama ikiendelea kuwa hivi ilivyo sasa, hatakuwa na jambo lingine zaidi ya kuomba msaada FIFA.

“Morrison amesema kuwa amewapa muda Yanga wa kuhakikisha kuwa wanamlipa fedha zake ambazo anadai, ingawa hajasema kuwa ni kiasi gani na fedha za nini.

“Kubwa amesema kuwa kama huo muda ambao ametoa hatolipwa ndiyo atakwenda FIFA ili aweze kupewa haki yake,” alisema mtu huyo.

Alipotafutwa Morrison mwenyewe ili kuweza kujibia taarifa hizo ilikuwa ngumu kumpata, ingawa mtu wake wa karibu alisema kuwa yupo Morocco kwenye klabu ya FAR Rabbat inayonolewa na Nasreedin Nabi akimalizia taratibu za kujiunga na timu hiyo.

Stori na Issa Liponda


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad