AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Watu 13 wanaaminika wamefariki dunia baada ya mitumbwi miwili waliyokuwa wakisafiria kuzama katika Ziwa Victoria wilayani Bunda mkoa Mara, ambapo jitihada za kutafuta miili zinaendelea.
Inahisiwa kuwa Mitumbwi hiyo ilikuwa imebeba watu 28, tukio hilo walipokuwa wakitoka Kijiji cha Mchigondo kwenda Kitongoji cha Bulomba, kuhudhuria ibada ambapo 14 waliokolewa wakiwa hai na mwili wa mtoto mmoja ulipatikana.
Kati ya Watu waliozama katika ajali hiyo ya majini, 11 ni wanafunzi wa Shule ya Msingi Igundu iliyopo Wilaya ya Bunda Mkoani Mara, huku ikidaiwa kuwa hali mbaya ya hewa ni moja kati ya sababu zilizokwamisha uokoaji.
Awali, Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dkt. Vicent Naano alisema, shughuli za uokoaji zilisimama kutokana na hali ya upepo na kwamba walikuwa wakifanya jitihada ili kufanikisha zoezi hilo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK