Mchezaji wa zamani wa timu za Gor Mahia na Sofapaka Aanguka na Kufariki Uwanjani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mchezaji wa zamani wa timu za Gor Mahia na Sofapaka Raphael Asudi ameripotiwa kuanguka, kuzirai na kufariki uwanjani wakati wa medhi mjini Thika kaunti ya Kiambu.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, Asudi alikuwa anashiriki katika mechi ya kirafiki baina ya timu za Donholm Seniors dhidi ya Thika Vitambi katika uga wa Thika Municipality wakati alianguka ghafla uwanjani mechi ikiendelea na kutangazwa kufariki dakika chache baadae.


Majaribio ya wachezaji wenzake na timu ya kiufundi ya kusimamia usaidizi wa matibabu ili kuokoa maisha yake yalishindikana.

Mpaka kifo chake, Asudi alikuwa na miaka 27 tu.

“Asudi alianguka katikati ya mechi na kusababisha hofu kwa wachezaji wenzake na wapinzani. Wajumbe wa benchi la ufundi na wachezaji wenzake walijaribu kutoa huduma ya kwanza kabla ya kukimbizwa hospitalini. Baada ya saa mbili, ilithibitishwa kuwa mchezaji huyo amepoteza maisha,” chanzo kimoja cha habari kiliripoti.

Asudi, kulingana na chanzo cha familia, alikuwa amefanyiwa upasuaji unaohusishwa na ugonjwa wa moyo. Inasemekana aliambiwa aache soka.

Ripoti zinaonyesha kuwa mchezaji huyo alitakiwa kusafiri hadi Hungary kwa masomo mwishoni mwa mwezi baada ya kupata ufadhili wa masomo.

Asudi pia alichezea vilabu vingine vya Ligi Kuu ya Kenya kama Sofapaka, Nairobi Stima, Posta Rangers na Bidco United.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad