Hatimaye Abby Chams 'Afunguka Marioo Hana Washauri Wazuri'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Hatimaye Abby Chams 'Afunguka  Marioo Hana Washauri Wazuri'

  Hatimaye Abby Chams 'Afunguka  Marioo Hana Washauri Wazuri'

Msanii wa Bongo Fleva, Abigail Chamangwana 'Abby Chams' amesema kuwa msanii wa Bongo Fleva, Omary Ally Mwanga maarufu kama Marioo hana washauri wazuri hasa kwenye kuchagua kipi cha kuzungumza hadharani na kipi si cha kuzungumza.


Abby Chams amesema hayo wakati akihojiwa na mtangazaji Alfred Bundala wa SNS kufuatia wawili hao kupishana mitandao kisa kikidaiwa kuwa Marioo kufuta verse ya Abby kwenye ngoma yake ya Love Song.


“Kulikuwa na hii ngoma ya Marioo, akanisikilizisha, ni nyimbo ambayo ni nzuri tukakubaliana tukaenda studio tukaifanya, nilirekodi verse yangu ya kwanza, na yeye akarekodi ya kwake ya pili lakini hakumalizia. Nilirudi nyumbani kama saa 12 alfajiri kwa sababu ilikuwa session ndefu, sijui kilichotokea.


“Kuna siku nikamcheki kumuuliza hii ngoma ni kali tutaimalizia lini, akasema atanicheki aniambie lini tutaimalizia. Siku moja nikaamka nikakuta ngoma imeshatoka, nilishangaa tu ikabidi niruhusu.


“Sio kweli kwamba nilikuwa siupendi ule wimbo, kama alinisikilizisha, nikaenda studio na tukaifanya kwa nini niseme sijaipenda, ule ulikuwa niliona kabisa ni wimbo mzuri. Sijui kwa nini alisema hivyo, labda kwa sababu ya kujitetea.


“Nilishtuka kusikia maneno aliyosema Marioo kwamba sina shukrani, yule ameshakuwa mtu mzima anajua kwamba akisema jambo kwenye public madhara yake ni makubwa na haitakiwi kisheria. Nadhani hana washauri wazuri," amesema Abby Chams.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad