AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mashabiki wa klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika ya Kusini, wamshambulia kocha wa klabu hiyo, Molefi Ntseki, baada ya kupoteza mchezo dhidi ya SuperSport United kwa bao 1-0 siku ya Jumatano.
Mashabiki hao waliojawa na ghadhabu walimrushia makopo ya maji Kocha, Molefi Ntseki aliyelazimika kutolewa uwanjani chini ya ulinzi mkali wa polisi wa kuzuia ghasia.
Hasira za mashabiki zilitokana na mwenendo mbovu wa klabu hiyo baada ya kupoteza michezo mitatu, huku ikiwa ni mara ya pili kwa mashabiki hao kumshambulia Ntseki, ambapo tukio kama hilo lilitokea wakati Amakhosi, walipopoteza dhidi ya TS Galaxy mwezi uliopita.
Kaizer Chiefs imefanikiwa kukusanya pointi 8 pekee kwenye mechi 7 ilizocheza, hivyo kujikuta nyuma kwa pointi 13 mbele ya vinara wa ligi hiyo, Mamelodi Sundowns.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK