Maxi Nzengeli Anabalaa Lake, Kiungo Huyu wa JKT Afunguka Jaramba Alilopigwa na Kijana Huyo Mdogo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Maxi Nzengeli Anabalaa Lake, Kiungo Huyu wa JKT Afunguka Jaramba Alilopigwa na Kijana Huyo Mdogo

Kiungo wa JKT Tanzania, Hassan Nassor Maulid ‘Machezo’ aliyesimama kati na kuchuana na Mudathir Yahya na Stephane Aziz Ki wa Young Africans katika mechi ya Ligi Kuu Bara na timu hiyo kupigwa mabao 5-0, amesema hakuna mchezaji aliyewanyimna raha kama Maxi Nzengeli aliyedai hakabiki uwanjani.

Timu hizo zilikutana mapema wiki hii kwenye Uwanja wa Azam Complex, huku Maxi akiendelea kutoa shoo ya maana akifunga mabao mawili na Machezo anasema licha ya kukabana na viungo wawili mahiri, Mudathir na Aziz KI, lakini aliyewatesa zxaidi ni Maxi.

“Mimi nilikuwa sina bato yoyote na Aziz Ki au Mudathir, nilichokuwa nafanya ni kutekeleza majukumu niliopewa na kocha, ila aliyetusumbua ni Maxi, kwani jamaa hakabiki kabisa,” amesema Machezo.

Amesema mara nyingi alikuvwa akijaribu kumkaba Maxi lakini hata ukimfanyia press unakuta keshatoa mpira mguuni kwake tofauti na wachezaji wengine

“Nikiri wazi kwamba aliyenipa tabu kwenye mchezo huo ni Maxi kwa sababu hata ukimfanyia press unakuta keshatoa mpira, ila kwa Aziz Ki nilimsoma vizuri alikuwa na chenga moja tu na Muda namuona wa kawaida, ndio maana namtaja aliyetusumbua, Maxi anajua sana,” amesema kiungo wa zamani wa Mbeya City.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad