Ajali yaua Watatu, Wanne Wajeruhiwa Pwani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Kibaha. Watu watatu wamefariki na wengine wanne wamejeruhiwa kufuatia ajali iliyohusisha magari mawili yaliyogongana uso kwa uso Kijiji cha Mbala Vigwaza mkoani Pwani usiku wa Oktoba 23, 2023.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Octoba 24, 2023 Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Pius Lutumo amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa gari dogo aina ya Toyota Kluger lililokuwa likitokea mkoani Iringa kuelekea Jijini Dar es Salaam

"Waliokuwa kwenye gari dogo walikuwa wanatoka Iringa kuelekea Dar es Salaam na huyu wa lori aina ya Scania alikuwa akitokea Dar es Salaam kuelekea mkoani Morogoro, lakini dereva wa gari dogo alikuwa na mwendo mkali bila kuchukua tahadhari," amesema.

Amewataja waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo kuwa ni pamoja na Mbuma anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka (35-40), Pokera (19) wote wakazi wa Mbezi Dar es Salaam na Mwanahamisi (18) mkazi wa Kijitonyama jijini humo.

Amewataja pia majeruhi kuwa ni pamoja na Amina Kondo mkazi wa Manzese Dar es Salaam, Abdallah Ally na majeruhi wawili ambao bado hawajatambulika majina yao.

Lutumo amesema kuwa miili ya marehemu hao imehifadhiwa kwenye Hospitali ya Lugoba na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu kwenye Hospital ya Msoga mkoani Pwani.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad