Kocha Gamondi Akemea Ubinafsi Young Africans

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kocha Mkuu wa Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans, Miguel Angel Gamondi, amewataka wachezaji wa timu hiyo kuacha kuangalia mambo binafsi haswa katika kushindania takwimu kwani jambo hilo litasababisha madhara makubwa ambayo hayatakuwa na msingi na tija ndani ya timu hiyo.

Gamondi amezungumza hayo kutokana na kuonekana wachezaji wake watatu ambao wanacheza katika eneo la kiungo kulingana kwenye idadi ya mabao ambao ni Maxi Nzengeli, Pacome Zouzoua na Stephane Aziz Ki.

Wachezaji hao wote watatu kwa pamoja wamefanikiwa kufunga mabao 9 kwenye Ligi Kuu Bara, ambapo kila mmoja akiwa amefunga mabao matatu.

Gamondi amesema kuwa anafurahi kuona wachezaji wake wakifunga mabao, lakini ametoa wito kwa wachezaji hao kucheza kwa faida ya kuisadia timu na si kuangalia mambo yao binfasi kwani itasabisha hasara kwa timu.

“Wachezaji wangu nimekuwa nikiwaeleza juu ya kuwaza kuisadia timu kwanza na wao baadae, hivyo nimekuwa nikiwasisitizia kama watakuwa wanataka kushindana wao kwa wao basi timu hii haitaweza kupata faida kubwa, najua wachezaji wanapotaka kila mmoja kutaka kuonesha kitu basi huo utasababisha uchoyo na hio ni mbaya.

“Nafurahi kwa kuwa viungo wangu wanacheza vizuri na wote wanafunga, lakini wanatakiwa kufahamu kuwa wanafanya haya kwa ajili ya timu kwanza na hayo mengine ni baadaye,” amesema kocha huyo kutoka nchini Argentina.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad