Kocha Gamondi Amekataa Kutoka Kileleni Ligi Kuu, Mechi Inayofuata Adai ni Fainali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Kocha Mkuu wa Young Africans, Miguel Angel Gamondi amesema kuwa hataki kuondoka katika kilele cha msimamno wa Ligi Kuu Bara huku akiuchukulia kila mchezo uliokuwepo mbele yake kama fainali.

Hiyo huenda ikawa salamu kwa Simba SC ambao wamepanga kuwapoka Young Africans taji la Ligi Kuu Tanzania Bara walilolichukua misimu miwili mfululizo wakiwa na Kocha Mkuu Mtunisia, Nasreddine Nabi.

Young Africans inaongoza katika msimamo wa ligi ikiwa na alama 18, ikifuatiwa na Simba SC yenye alama 15 na leo itashuka dimbani kucheza dhidi ya Ihefu FC.

Gamondi amesema kuwa amekaa na wachezaji wake na kumsisitiza kila mchezaji atakayepata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza anatimiza vema majukumu yake ya uwanjani.


Gamondi amesema ubingwa wa msimu huu hautakuwa mwepesi tofauti na misimu iliyopita kutokana na kila timu kuipania Young Africans, kwa kucheza kwa bidii kwa lengo la kutaka kuwafunga.

Ameongeza kuwa ameliona hilo mapema, na kuwataka wachezaji wake kila mchezo kucheza kama fainali, kwa lengo la kupata pointi tatu ili malengo yao yatimie ya kutetea taji hilo.

“Hatutaidharau timu yoyote tutakayokutana nayo katika ligi, ni kutokana na kila timu inabadilika inapokutana dhidi ya Young Africans, inatumia nguvu nyingi kwa kucheza kwa kutupania, kwa lengo la kutufunga.

“Kama kocha nimechukua tahadhari mapema ya hilo, kwa kuwataka wachezaji wangu wanacheza kila mchezo wa ligi kama fainali kwa lengo la kupata pointi tatu zitakazotubakisha kileleni katika msimamo.

“Ninataka kuona tukipata ushindi katika kila mchezo utakaokuwepo mbele yetu, nimewasisitiza juu ya hilo wachezaji wangu wote kwa kuanzia mchezo wetu wa jana dhidi ya Singida Big Stars,” amesema Gamondi.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad