Ally Kamwe : Yanga Tunakwenda Kuonesha Dunia Jinsi Gani Tunamfunga Al Ahly

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ally Kamwe : Yanga Tunakwenda Kuonesha Dunia Jinsi Gani Tunamfunga  Al Ahly



Baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Simba SC, uongozi wa Young Africans umesema kuwa sasa ni zamu ya Mabingwa wa Soka Barani Afrika Al Ahly ya Misri kuhakikisha kuwa wanapokea kichapo kutoka kwao katika michezo ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika pindi watakapokutana.

Young Africans watakutana na Al Ahly katika michezo ya Ligi ya Mabingwa Afrika Kundi D ambalo linawajumuisha vigogo hao wawili pamoja na CR Belouzdad kutoka Algeria na Madeama kutoka Ghana.

Ofisa Ally Kamwe alisema: “Baada ya kuwafunga Simba SC sasa tunataka kwenda kuionyesha dunia ni namna gani Young Africans tutamfunga Al Ahly ambao walishindwa kufungana na Simba SC katika michezo waliyokutana nao.

Young Africans msimu huu tumedhamiria na tunataka kuhakikisha kuwa tunafika mbali katika michuano hii ya kimataifa ambayo watu wanatuona kama hatuwezi kufanya kitu.

“Tuna malengo makubwa ambayo tutawaonyesha watu baada ya kufanikiwa, kwa sasa hatutaki kuongea sana kwa kuwa watu hawawezi kutuelewa lakini Young Africans hii niwahakikishie mashabiki wetu kuwa watafurahi sana,” amesema Kamwe.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad