AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kamati ya nidhamu ya shirikisho la soka barani Afrika Caf imemfungia kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Adel Amrouche mechi 8 kwa kutoa kauli ambazo zimetafsiriwa kama ni kauli za uchochezi.
Siku moja kabla ya mchezo wa kwanza dhidi ya Morocco kocha Adel aliwatuhumu Morocco kwamba wao ndio wanaouendesha mpira wa Afrika kwa kuamua wacheze muda gani, waamuzi wa mechi zao na kupanga ratiba za michezo yao.
Kauli hiyo ilikanushwa na TFF kupitia Rais Wallace Karia kuwa kauli hiyo ni ya kocha na sio ya TFF.
Chama cha soka cha Morocco kilipeleka malalamiko Caf kwa kauli hizo hali ambayo ililazimisha kamati ya nidhamu kukutana na kutoa adhabu ya kumfungia mechi 8 huku akipewa siku tatu za kukata rufaa.
Kwa kufungiwa kwa kocha Amrouche sasa ni wazi kocha Hemed Moroko na Juma Mgunda.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK