Fei Toto Awakataa Mashabiki wa SOKA...."Sishindani na Mtu Uwanjani"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Fei Toto Awakataa Mashabiki wa SOKA...."Sishindani na Mtu Uwanjani"

Kiungo kutoka visiwani Zanzibar na Klabu ya Azam FC, Feisal Salum ‘Fei Toto’ amesema kila anachokifanya uwanjani ni kwa ajili ya timu yake na anapofunga hakuna anayeshindana naye, bali ni kuipa matokeo mazuri timu yake.

Nyota huyo amesema anafurahi kuona anaisaidia zaidi timu yake kuweza kupata matokeo mazuri katika kila mchezo.

Azam FC leo Alhamis (Mei 09) imeshuka uwanjani kuumana na Simba SC kwenye mfululizo wa michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayokwenda ukingoni.

“Kila ninachokifanya uwanjani ni kwa ajili ya timu yangu, sichezi kwa kushindana na mtu, nacheza kuisaidia timu kufanya vizuri, nashukuru Mungu kwa kila kitu kizuri ninachokifanya kwa ajili ya timu, ushindi tunaopata niwe nimefunga mimi au mtu mwingine unatokana na jitihada na juhudi za wachezaji wote,” amesema Fei Toto.

Fei Toto mpaka sasa ameifungia timu yake mabao 15 na kutoa pasi za magoli ‘asisit’ saba akilingana na kiungo wa Young Africans, Azizi Kii.

Mashabiki wa soka nchini tayari wameanza kuwashindanisha nyota hao kutokana na kasi yao ya kufunga huku wakiwa wamelingana idadi ya mabao ya kufunga na wanaamini mfungaji bora msimu huu atatoka kati yao.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad