Kasi ya Kimbunga Hidaya yaimarika Hadi Kilomita 110 Kwa saa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kasi ya Kimbunga Hidaya yaimarika Hadi Kilomita 110 Kwa saa


Mienendo ya mifumo ya hali ya hewa baharini bado inaonyesha uwezekano mkubwa wa Kimbunga Hidaya kuendelea kusogea karibu na pwani ya Tanzania na kuendelea kuwepo hadi tarehe sita mwezi Mei 2024, kwa mujibu wa Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania TMA.


Kulingana na mamlaka hiyo, kimbunga hicho kinaendelea kuimarika na kwamba hadi kufikia usiku wa kuamkia leo kasi yake ilikuwa imeimarika na kufikia kilomita 110 kwa saa.


Taarifa hiyo inasema kwamba kimbunga hicho kitaendelea kuimarika na kuwa kikubwa zaidi katika saa 24 zijazo.


Imesema kwamba uwepo wa kimbunga hicho katika pwani ya Tanzania utavuruga mifumo ya ali ya hewa nchini na kusababisha mvua kubwa na upepo mkali.


Baadhi ya maeneo yatakayoathirika sana ni Mikoa ya Mtwara, Dar es Salaam, Lindi, maeneo ya Tanga, Morogoro , visiwa vya pemba na Unguja pamoja na maeneo Jirani.


Taarifa hiyo imeongezea kwamba tayari vipindi vya mvua nyepesi na upepo wa wastani vimeanza kujitokeza katika maeneo ya Mtwara.


TMA imesema kwamba ongezeko la mvua na upepo mkali utakaoambatana na mawimbi makubwa baharini vinatarajiwa kusambaa katika maeneo mengi ya ukanda wa pwani kuelekea tarehe 4 hadi 6 mwezi Mei 2024.


Kutokana na hilo, TMA imetoa tahadhari kwa wananchi katika maeneo husika na wote wanaojihusisha na shuguli mbalimbali baharini .


VIlevile Mamlaka hiyo imewataka Watanzania kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiriwa hali ya Hewa.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad