AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
TABIA ya baadhi ya mastaa kuonyeshaonyesha bastola hadharani kimemtokea puani ‘memba’ wa Kundi la Tip Top Connection, Khalid Ramadhani ‘Tunda Man’ baada ya hivi karibuni kuitwa na jeshi la polisi na kuhenyeshwa.
Akizungumza na GPL hivi karibuni Tunda Man alisema makala iliyotoka kwenye gazeti ndugu na hili la Ijumaa Wikienda ikieleza jinsi baadhi ya wasanii wanavyozianika silaha kiholela imemfanya akione cha moto kwani wakati akizungumza na mwandishi wetu alikuwa Kituo cha Polisi cha Kati (Central) akihojiwa.
“Kwanza naomba nikwambie kuwa hakuna kitu ambacho kimenikosesha amani leo (Jumatatu) kama hii habari yako uliyoandika kwenye gazeti, hivi ninavyoongea na wewe niko ‘sentro’ nikihojiwa, kiukweli sina amani,” alisema Tunda Man.
Hivi karibuni msanii wa muziki, Aboubakar Chende ‘Dogo Janja’ alinaswa akiwa na bastola na alipoulizwa ni ya nani alidai ni ya Tunda Man hivyo kumpa msala mwenzake.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK