KIGOGO ALIYEFUKUZWA CCM AFICHUA SIRI NZITO

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

HATIMAYE Mwakilishi wa Kiembesamaki, Mansour Yussuf Himid, aliyevuliwa uanachama na vikao vya juu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma, ameibuka na kutoa kauli nzito dhidi ya chama hicho huku akitoa siri ya kutimuliwa kwake.

Akizungumza kwa mara ya kwanza tangu alipotimuliwa katika kongamano  la wazi lililofanyika kwenye Ukumbi wa Bwawani mjini hapa jana, Mansour alisema licha ya kuvuliwa uanachama hataacha kutetea masilahi ya Zanzibar bila woga.

Waziri huyo wa zamani na aliyekuwa Mwakilishi wa Kiembesamaki, alifichua siri kuwa alianza kujengewa chuki, fitina na viongozi wenzake  baada ya kuonekana mtetezi na mpigania masilahi ya Zanzibar, ukiwamo msimamo wake wa kutaka  suala la mafuta na gesi asilia liondoshwe kwenye orodha ya mambo ya muungano.

Mwanasiasa huyo mwenye ushawishi mkubwa katika siasa za Zanzibar, alisema amepokea uamuzi huo kwa moyo mweupe na hatarajii kwenda mahakamani au  kuwania tena uwakilishi wa jimbo hilo kupitia chama chochote.

“Nimekubali kufukuzwa uanachama na NEC ya CCM, wenzako kama hawakutaki huna njia ya kujipendekeza kwao, sitakwenda kortini wala sihitaji kugombea kwa chama chochote cha siasa,” alisema Mansoor.

Hata hivyo alisisitiza kuwa licha ya kufukuzwa, ataendelea kutetea masilahi ya Zanzibar bila woga na hatanyamazishwa kwa vile hiyo ni haki yake kikatiba kama raia huru, pia kadi yake ya CCM haikuwa kimeo kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.

Mansoor alisema lengo la Mapinduzi ya Zanzibar  ya mwaka 1964 ilikuwa kutafuta ukombozi na uhuru wa kifikra, kiuchumi na kidemokrasia na si kufunga au  kuzuia mawazo na maoni ya watu.

Mwanasiasa huyo mwenye ushawishi katika siasa za Zanzibar, alisema kuwa alianza kujengewa kinyongo na viongozi wenzake  baada ya kuonekana kuwa ni mtetezi na mpigania masilahi ya Zanzibar, ukiwamo msimamo wake wa kutaka  suala la mafuta na gesi asilia liondoshwe kwenye orodha ya mambo ya muungano.

“Hapa ndipo nilipoanza kuonekana mnoko, nikapewa majina mengi na kupigwa. Kwa taarifa yao, sitaacha kupigania ninachokiamini, nitabaki kuwa mtetezi wa haki na usawa hadi nitakapokufa,  ila sihitaji kuwa mwakilishi wa mahakamani, sina pesa ya kulipa wanasheria, mshahara wenyewe umekatwa miguu,” alisema Mansoor huku nyimbo za kimapinduzi zikiimbwa ukumbini.

Alisema kitendo cha CCM kumpima na kumuona hafai ni haki yao na ataendelea kuheshimu maamuzi hayo, kwa sababu ndiyo yaliyotolewa  na kufikiwa na chama kwa kufuata taratibu zao.

Alisema  malengo  yake mengi ya kisiasa akayaweka wazi ifikapo mwaka 2015 kama ataona kuna haja ya kufanya hivyo, lakini alisisitiza kuwa hataiacha  au kuitupa  Zanzibar katika maisha yake akiwa ndani au nje ya chama chochote.

Akizungumzia muungano, mwanasiasa huyo alisema yeye ni muumini wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar lakini alisema kuwa angependa kuona muungano wenye usawa, haki na heshima na si upande mmoja kuutafuna mwingine.

Kwa upande mwingine alisema kuna baadhi ya vyama  vya siasa vimeanza kumfuata na kumtaka awe mwenyekiti wa taifa na wengine wakitaka achukue fomu ya kuwania kiti cha Kiembesamaki.

Alilaumu tabia na hulka ya baadhi ya wanasiasa wa Zanzibar kupenda kubaguana kwa rangi na uzawa na kuongeza kuwa mambo hayo si mazuri kuyakumbatia kwani hayana mwisho mwema.

Wakati huo huo, Kamati ya Maridhiano Zanzibar imekiri kuwa haina tena  uwakilishi wa vyama vya siasa vya CCM na CUF.

Msimamo huo  kwa mara ya kwanza umewekwa  wazi jana na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hassan Nassor Moyo.

Moyo alisema kuwa kamati yake ni ya utetezi na kupigania masilahi ya Zanzibar na kazi yake kubwa ni kudai hadhi na tunu ya Zanzibar kama nchi na taifa lenye mamlaka na uwakilishi  katika Umoja wa Mataifa.

Msimamo huo umekuja baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, kuikana hadharani kamati hiyo na kusema haitambui na wala haina baraka za CCM wala serikali yake.

Katika kuonesha kuwa kamati hiyo ni ya wananchi, hata Mratibu wa kongamano hilo ambaye pia ni Mwakilishi wa Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu, alipokuwa akimkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria wa SMZ, Aboubakari Khamis Bakari, alisisitiza kuwa anasimama kuchangia na kutoa  maoni yake kama mwananchi na si kwa kofia ya dhamana yake.

Akizungumza katika kongamano hilo, Waziri wa Katiba na Sheria Zanzibar, Aboubakar Khamis Bakari, alisema rasimu ya mabadiliko ya katiba haifai kwa vile inainyima Zanzibar mambo mengi ya msingi na kuikandamiza kiuchumi.

Aboubakary alisema muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa mataifa mawili yaliyokuwa na uwakilishi sawa kama dola, hivyo si haki upande mmoja kuonekana mgeni mwalikwa katika ushiriki wake.

Aliwataka wananchi kuacha hofu ya kuwapo kwa muungano wa serikali tatu na kusema jambo hilo halitavunja muungano au kutokea machafuko.

Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Maridhiano, Eddy Riyami, alitangaza kuhama rasmi CCM na kusema ataamua baadaye atajiunga na chama gani kama ataona kuna haja ya kufanya hivyo.

Riyami alichukua mjadala mkubwa wakati wa sakata la kutoweka  na kujiuzulu kwa aliyewahi kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Mkunazini, Salum Msabaha Mbarouk, ambaye sasa amehamia CCM.

Source:Tanzania Daima
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad