SABABU ZA (KAGAME) RWANDA KUIKACHA BANDARI YA DAR HIZI HAPA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

SIRI ya wateja wakubwa wanaotumia Bandari ya Dar es Salaam, wakiwemo wa nchi jirani kama Rwanda kutishia kujitoa na kwenda kutumia bandari za nchi nyingine, imefahamika, Tanzania Daima Jumapili limebaini.

Siri hiyo inaelezwa kusababishwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kuwa na mpango wa kuanzisha tozo mpya kuanzia Oktoba mwaka huu kwa wateja wanaoingiza mizigo yao nchini pamoja na kasi ndogo ya utendaji ukilinganisha na bandari za nchi jirani.

Tozo hiyo mpya inayopigwa ni ya ufuatiliaji mizigo bandarini kwa njia ya mtandao (Electronic Cargo Tracking Note).

Hatua ya Rais Kagame kuikacha Bandari ya Dar es Salaam kunadaiwa kusababishwa na kulegalega kwa mahusiano kati ya Tanzania na Rwanda, lakini duru za siasa zinabainisha kuwa rais huyo alishaitahadhalisha serikali kuboresha utendaji wa TPA na kupunguza vikwanzo vya kibiashara kutoka 24 hadi 12.

Imeelezwa kwamba tozo hiyo ya e-CTN itaathiri mapato ya bandari za Tanzania kutokana na kuwa washindani wake wote hawana tozo hizo ikiwamo bandari za Mombasa, Walvis bay, Nacala, Maputo na Durban, ambazo zimekuwa zikichukua wateja wengi wa bandari za Tanzania wakiwamo wale wa nchi za Burundi, Rwanda, Zambia, DRC na Malawi.

Vyanzo vya habari vimeeleza kuwa kodi hiyo imeibua utata mkubwa baada ya kuwapo njama za kulazimisha kuwapo kwake pamoja na pingamizi kutoka kwa wadau na hata baadhi ya watendaji serikalini.

Taarifa za uhakika ndani ya mfumo wa bandari zilizothibitishwa na baadhi ya wadau, zinaeleza kwamba TPA ambao wamekwisha kuingia mkataba na kampuni moja ya Ubelgiji, iitwayo Antaser BVBA imeendelea na mchakato wa kuanzisha tozo hiyo.

Pamoja na pingamizi kutoka kwa wadau na hata ndani ya TPA yenyewe, bado kuna taarifa za kwamba uongozi wa mamlaka hiyo unaendelea na mchakato wa kuanza tozo hiyo ya e-CTN Oktoba mosi mwaka huu na baadhi ya watendaji wake wanapanga kwenda Ubelgiji kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya utekelezaji wake.

Tozo hiyo ya e-CTN ni kwa ajili ya ufuatiliaji wa mzigo kutoka nchi inakotoka kwa njia ya mtandao, kazi ambayo wadau wanasema hufanywa na kampuni za meli na zile za wakala wanaosafirisha mizigo hiyo na si dhamana ya TPA ambao jukumu lao ni kupokea mizigo kutoka kwenye meli (cargo handling) na kuifadhi kwa muda ikisuburi wateja kuichukuwa.

“TPA walitakiwa wawasilishe pendekezo hili la e-TCN kwa Sumatra ambao kwa mamlaka waliyonayo wawaite wadau wote watoe mapendekezo yao kama uwepo wa kitu kama hiki utaleta tija kwa wadau wote wanaotumia bandari ya Dar es salaam. Kutokana na hila na pengine ufisadi uliojificha ndani. Gharama zake zitakwenda kwa mlaji wa mwisho!  TPA kazi yake ni kupokea mizigo kutoka kwenye meli (Cargo handling) na kuifadhi kwa muda ikisuburi wateja waje kuichukuwa aidha wao wenyewe au kwa kutumia mawakala wao wa forodha.

“TPA wanatakiwa ku kuibana  mizigo ikiwa ndani ya bandari na si kutoka bandari nyingine duniani ( ports of loadings) mpaka final destination ya mizigo bila " carriers" yaani shipping lines/ agents kuhusika na pia wenye mizigo (Cargo Owners) yaani importers/ C&F agents kuhusishwa!!.  Hapa kuna kitu kilichojificha,” anasema mdau ambaye anafanya biashara ya uwakala wa meli.

Tayari kumeibuka utata kuhusiana na huo mradi wa Electronic Cargo Tracking Note baada ya wadau kushitukia njama za kuwazunguka kwa njia ya kughushi muhstasari wa kikao wenye nia ya kuhalalisha mradi huo.

Utata huo umeibuka baada ya wadau kubaini kuwapo kwa kikao kilichofanyika Mei 30, 2013 kikiwashirikisha baadhi yao na baadaye kuandika muhstasari (nakala tunayo) ambao uliandikwa majina ya watu ambao hawakuhudhuria akiwamo Mwenyekiti, Otieno Igogo.

Igogo alibaini kuwapo kwa njama hizo na baadaye ‘kuvamia’ kikao kingine kilichoitishwa bila ya yeye kualikwa kilichofanyikia Agosti 29, 2013, ambacho alikiongoza na kutamka wazi kuwa jina lake pamoja na baadhi ya hoja za kikao cha Mei 30, 2013 vilighushiwa na hivyo kwa kauli moja wajumbe kufanyia marekebisho muhtasari.

Miongoni mwa hoja zilizoghushiwa katika muhtasari wa kikao hicho ni hoja ya kwamba wajumbe walijadili na kuridhia mpango wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kuanzisha tozo kwa ajili ya huduma za Electronic Cargo Tracking Note (e-CTN), na katika kikao cha wiki hii, wadau walirekebisha muhtasari huo na kukemea waliohusika na kughushi.

Mwakilishi wa Chama cha Mawakala wa Meli (TASAA), Paul Kirigini, ambaye ni mjumbe wa vikao hivyo alithibitisha kuwapo kwa tatizo katika muhtasari wa kikao cha Mei 30, 2013 ambao uliandaliwa katika mazingira tata kwa kuorodhesha watu ambao hawakuhudhuria na baadhi kuandika kwamba waliomba udhuru wakati hawakuwa wamealikwa akiwamo yeye.

“Mimi sikualikwa lakini wameandika kwamba sikuhudhuria kwa kuomba udhuru. Nilikuwapo Dar es Salaam na hata kama nisingekuwapo tungetuma mwakilishi wa TASAA, lakini hawakutuita na wakaandika kwamba tuliomba udhuru. Kibaya zaidi hata Igogo ambaye alipaswa kuwa mwenyekiti wa kikao hicho hakuwapo lakini wakaandika ndiye aliendesha hicho kikao,” anasema Kirigini.

Igogo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Wadau wa Bandari,  hakuweza kupatikana jana kuzungumzia sakata hilo, lakini ilielezwa kwamba ameridhika baada ya muhtasari huo kufanyiwa marekebisho na kuazimiwa kwamba vikao vyote lazima wadau wajulishwe kabla ya kuitishwa.

Mjumbe mwingine ambaye anatajwa jina lake kuingizwa bila ya yeye kuwapo ni Stephen Ngatunga, ambaye naye aliomba kufanyika kwa marekebisho hayo katika kikao cha Alhamisi wiki hii.

Mwakilishi wa TPA, ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Teknohama, Phares Magesa, anaelezwa kuwa ndiye aliyemuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wake, Madeni Kipande, ambaye hata vikao vilivyoitishwa na SUMATRA alishindwa kuhudhuria.

Mara baada ya kutokea malalamiko kuhusiana na Electronic Cargo Tracking Note, wadau walilazimisha kuitishwa kwa kikao kilichoongozwa na SUMATRA, lakini uongozi wa TPA ulishindwa kuhudhuria vikao vilivyoitishwa Julai 17 na Julai 22 mwaka huu.

Katika vikao hivyo viwili vya Julai, SUMATRA iliungana na wadau kuitaka TPA kuwashirikisha kabla ya kufikia maamuzi ya kuingiza tozo zozote zitakazoweza kuathiri wateja wanaotumia bandari za Tanzania ikiwamo bandari ya Dar es Salaam.

Mradi huo wa e-CTN unaelezwa na wadau kuweza kupandisha gharama za uingizaji wa mizigo bandarini hadi kufikia dola milioni 100 kwa mwaka kwa kutumia takwimu za mizigo ya makontena kwa mwaka 2012, ukiondoa mizigo mingine kama magari, nafaka na mafuta.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ameshaingilia kati changamoto ndani ya Bandari ya Dar es Salaam na aliitisha kikao cha wadau kilichoahirishwa ghafla kutokana na kuingiliana na majukumu mengine ya kitaifa.
Tanzania Daima
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad