SUMAYE ALITAKA BUNGE KUFUTA TAKRIMA SEREKALINI...WENGI WANATUMIA KAMA KICHAKA CHA KUFICHA MAOVU YAO

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


  Alishauri Bunge kuibadili sheria `aliyoiasisi`
  Asema inatumika kama kichaka cha rushwa
  Asisitiza ilitungwa kwa wema, sasa inakiukwa
Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye
Msemo wa sheria ni msumeno, umedhihirika sasa kwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ambaye anataka sheria iliyohalalisha matumizi ya takrima kwenye uchaguzi ifutwe.
 Sheria hiyo iliyopitishwa miaka ya 2000, ilitungwa na Bunge lililoongozwa na Spika Pius Msekwa, wakati Sumaye akiwa Waziri Mkuu na Kiongozi wa shughuli za serikali bungeni.
Aliyasema hayo wakati wa hafla ya kuzindua album ya waimbaji wa kwaya zilizo chini ya Umoja wa Vijana wa Kipentekoste katika vyuo vikuu (UPSF) vilivyopo mjini Morogoro jana, ambapo alikuwa mgeni rasmi.
Kwa mujibu wa hotuba yake iliyopatikana kwa njia ya mtandao, Sumaye alisema kumekuwapo matumizi mabaya ya takrima hasa wakati wa uchaguzi, akisema inachochea rushwa. “Leo sote tu mashuhuda wa neno takrima kutumika kama kichaka cha kujifichia wala rushwa,” alisema.
Aliongeza, “sheria zote hutungwa kwa malengo mazuri, lakini katika matumizi yake likijitokeza tatizo ambalo halikutegemewa, basi sheria hiyo hufanyiwa marekebisho au kufutwa kabisa.” 
Sumaye alisema, “ni vizuri Bunge letu tukufu sasa likaifanyia sheria hiyo marekebisho kwa kuliondoa kabisa neno takrima au kuipa tafsiri na ufafanuzi ulio wazi zaidi, ili wala rushwa wasiitumie takrima kama kichaka cha kujifichia.”
AKEMEA MAUAJI YA OPERESHENI
Sumaye, amekemea mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola, dhidi ya raia wasiokuwa na hatia ikiwamo kupitia operesheni zinazolenga kudhibiti uhalifu nchini.
Sumaye alisema, upungufu wa maadili mema ni tatizo kubwa katika jamii hivyo ipo haja ya kuweka misingi imara ya kuondokana na tatizo hilo.
Leo kuna mauaji ya kutisha yanayotokea bila sababu zinazotosheleza, kama vile watu kujitoa mhanga na kuua watu wengi wasio na hatia,” alisema.
Alitoa mfano akisema, “hapa kwetu tumeshuhudia watu wakiteketeza familia nzima kwa sababu tu kakosana na mpenzi wake, vyombo vya serikali kufanya mauaji wakati wanafanya operesheni mbali mbali jambo ambalo wanajua ni makosa.
MISINGI YA HAKI
Sumaye alisema wapo Watanzania wengi wanaoshindwa kupata haki zao mpaka `kutoa chochote’, wakiwamo madereva barabarani wanaopata shida kupita bila kuwahonga baadhi ya askari wa usalama barabarani.
Na haya yapo katika sehemu na sekta nyingi nchini. Ninapozungumza haya sijawahi kusema hata siku moja kuwa rushwa hii imeanza sasa na huko nyuma haikuwepo. La hasha! Rushwa imekuwepo hata kabla ya uhuru na imeendelea kuwapo hadi leo,” alisema.
Aliongeza, “hata  Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikiri kuwa hata wakati wa utawala wake rushwa ilikuwepo ila walikuwa hawana utani katika kukabiliana nayo.
Alisema ipo haja kukubali kuwa rushwa ni tatizo linaloongezeka kwa kasi, linaumiza uchumi wa nchi, wananchi na kuvunja heshima na hadhi ya taifa kwa jumuiya za kimataifa.
AOMBA RADHI
Hata hivyo, Sumaye aliomba radhi kwa kauli aliyonukuliwa Novemba 24, mwaka huu mjini Moshi, akisema Tanzania inaongoza kwa rushwa katika Afrika Mashariki.
Hapo niliteleza ulimi naomba radhi kama kuna waliokwazwa na hilo. Nilichotaka kusema ni kuwa “rushwa ni tatizo linaloongoza Tanzania katika kuathiri maisha ya watu wengi,” alisema.
 AWAASA VIJANA
Aliwaasa vijana kujiandalia maisha yatakayowawezesha kuchagia mabadiliko chanya katika kuwapo utawala bora na kupiga vita maovu, kuimarisha uchumi.
Aliyataja mabadiliko mengine kuwa ni katika kupiga vita umasikini, kustawisha ulinzi na amani.
Sumaye alisema, “kwa maoni yangu wasomi wetu hamjachukua nafasi yenu katika nchi na labda hata katika jamii. Kuna mambo mengi makubwa yanayotokea katika nchi lakini wasomi mnakaa kimya halafu yakisha haribika tunatafuta wa kuwanyooshea vidole,” alisema.
Aliongeza, “tuna maprofesa waliobobea wa fani mbali mbali, madaktari wahadhiri na wanachuo wanaoweza kutufanyia uchambuzi na utafiti ili kuwa na mchango chanya katika jambo lolote. Nafasi hii haijatumika ipasavyo na wakati mwingine hata nahisi imetumika vibaya.”
Alisema wanataaluma hao hawapaswi kuwaachia wanasiasa kila kitu pasipo kukosoa na kuonya, badala yake kuwa mithili ya watazamaji na baadaye walalamikaji.
AIPONGEZA UPSF
Alisema UPSF ina umuhimu kwa jamii kwa sababu, pamoja na mambo mengine, inawajenga vijana kiroho ili wawe watu wenye hofu ya Mungu.
Awali Mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi wenye imani wa makanisa ya Pentekoste Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA), Vicent Komba, alisema umoja huo haufungamani na upande wala taasisi ya dini yoyote bali upo kwa ajili ya kubadilisha watu kwa njia ya maombi na elimu kuweza kumrudia Mungu.
Alitaja baadhi ya mambo ambayo umoja huo umekuwa ukipambana nayo kuwa ni kuwabadilisha watu wanaojihusisha na madawa ya kulevya, pombe, ukimwi na masuala ya kifisadi ambayo yamekuwa ni tatizo kubwa hapa nchini na kusababisha madhara kwa kundi kubwa la vijana.
Alisema kuwa hali hiyo pia imekuwa ikisababisha taifa kukosa viongozi bora na wasio kuwa na maadili katika kuwatendea watu haki hivyo kupitia umoja huo watahakikisha wanarudisha uhusiano chanya baina ya viongozi na wananchi ili kuleta amani.
Walimhakikishia Sumaye kuwa watakuwa naye bega kwa bega kwa kumfanyia maombi ili kila kukicha wale wanaokusudia kumfanyia mabaya wasifanikiwe na yale anayokusudia kuyafanya katika siku zake za usoni yafanikiwe baada ya kuona mambo mazuri aliyofanya wakati wa uongozi wake alipokuwa madarakani.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kafulia 2015 hamhusu

    ReplyDelete
  2. Huwezi kuwa rais ww fisadi ulietukuka

    ReplyDelete
  3. urais mtamu!!!!!!!!!!!!!!!!!??????????????

    ReplyDelete

Top Post Ad