KWA WADADA:DALILI ZA MWANAUME ANAYEKUPENDA KWA DHATI

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

ANAVYOKUTAZAMA
Mwanasaikolojia Zick Rubin kutoka Chuo cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema kwamba watu wanaopendana hutumia asilimia 75 kutazamana kuliko wasiopendana, ambao kiwango chao ni asilimia 30-50. 

Hii ina maana kwamba mwanaume anapotumia muda wake mwingi kumtazama msichana na kugeuka taratibu kuangalia vitu vingine kama mtu asiyependa kuacha kumwangalia, ujue anampenda.

MIPANGO 
Mwanaume anayekupenda atakushirikisha kwenye mipango yake hasa ya muda mrefu. Mfano akitaka kununua kiwanja, kujenga nyumba atakuambia na pengine kutaka mchango wako wa hali na mali katika kulifanikisha hilo. Ukiona mwanaume anakuficha mambo yake, tambua kuwa huyo ana walakini kwenye penzi la dhati na la muda mrefu.

ATAONESHA HUZUNI
Katika maisha ya mapenzi kuna wakati wa kuhuzunika. Mwanaume mwenye upendo wa dhati atashirikiana nawe wakati wa huzuni na kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa unapata furaha. 





ATAKUAMINI
Dalili nyingine ya kupendwa na mwanaume ni kuaminiwa kwenye maisha kwa ujumla. Yaani mwanaume anayekupenda hatakuficha kitu, mfano pesa zake, atakupa uhuru kwenye simu yake na kukuamini katika usimamizi wa miradi yake.

ATAKUPA NAFASI
Ninapozungumzia nafasi nina maana atakukaribisha kwake bila hofu na kukupa nafasi ya kuingia na kutoka bila mipaka, atakupa nafasi ya kuweka vitu vyako kwenye kabati na kuruhusu nguo, picha na vitu vyako kuonekana wakati wote chumbani kwake.

UTAKUWA MWANAFAMILIA
Mwanaume aliyefikia chaguo la mwisho kwa mwanamke humshirikisha mpenzi wake kwenye masuala yake ya kifamilia, mfano atamwalika kwenye vikao vya harusi, kipaimara, atatoa nafasi ya kuambatana naye kuona wagonjwa, kusalimia ndugu na atakuwa huru kukutambulisha kwao.

ATAZUNGUMZA NAWE KUHUSU WATOTO
Kwa kuwa wanaume wengi hufikiria kuwa na familia, mwanaume anayekupenda atazungumza nawe mipango ya kupata watoto kwa kuwa atakuwa amekuchagua wewe kuwa mama wa wanaye na atapenda mazungumzo hayo.

ATAKUSAIDIA
Kwa kuwa kukwama ni sehemu ya maisha yetu, mwanaume anayekupenda atakuwa tayari kukusaidia unapokwama. Kila mara atahakikisha kuwa unakuwa na mafanikio na yeye atakuwa tayari kukupunguzia usumbufu wa maisha, kwa kukufuata kazini, kukusaidia baadhi ya mambo na hata ya nyumbani.

ATAJITOLEA
Ninaposema kujitolea ninamaanisha atakuwa tayari kufanya mambo yako na kuyaweka yake nyuma. Kwa mfano akiwa anapenda mpira na siku hiyo kuna mechi, lakini muda huo ukamwambia akufuate kwa mjomba wako atakuwa tayari kuacha furaha yake na kukujali wewe. Huyu ni mwanaume anayekupenda kwa dhati.

ATAAMBATANA NAWE
Wapenzi wengi wasiokuwa na mapenzi ya dhati huona aibu kuambatana na wapenzi wao kwenye mikusanyiko ya watu, lakini mwanaume anayekupenda atafurahia kutoka moyoni kuongozana nawe kwenye halaiki ya watu na kufurahia uwepo wako bila kuona aibu.

KAMA UMEIPENDA MADA NA KUKUSAIDIA, TUPIA BASI LIKE NIKUPAKULIE NYINGINE!!!!
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

11 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hivyo kama unahitajika kwenda kukagua ujenzi wa nyumba utaacha kwa sababu mwanamke anataka umsindikize saloon!

    ReplyDelete
  2. Sio kwel hayo yote mtu anaweza kupretend

    ReplyDelete
  3. Mengi ni yamsingi mpendwa wako

    ReplyDelete
  4. Mengi ni yamsingi mpendwa wako

    ReplyDelete
  5. Uko sahihi.nimeipenda

    ReplyDelete
  6. Ww ulie leta huu upuz umebugi tu kwenye mpira mm cwez kuacha kuangalia mpira eti nimfuate yy.acha usenge

    ReplyDelete
  7. Wewe unasema aache usenge si umezoea kufunua na kuacha ndo maana Hujui Penzi la dhati Swine wewe

    ReplyDelete
  8. Mwandishi acha kuwapoteza wakina hawa. Ee bhana cku hizi mchizi azime mwenyewe tu hainaga fomula kwani vyote ulivyoandika wa2 wanafanya. Kuna maduu mbuzi sana hawavuliki chupi sasa hao nakuongezea TIP nyingine huwa tunawaendeaga mpaka chachi babaako naitwa Petro nikimvua chupi naendelea kuwa Juma, TAHADHARI ! Wadada mume mwema hutoka kwa MUNGU mkiweka vigezo vyenu mtachemka.

    ReplyDelete
  9. Nimeipenda hii mada,usemavyo no kweli hats nami yashawahi kunikuta.

    ReplyDelete
  10. Tunaitaji sana kumshilikisha "MUNGU" kupata ndoa ya kweli alafu akili ye2 ndio inafuata

    ReplyDelete
  11. mie akinisaidia tu inatosha hayo mengine yatafata taratibu. maana hawa wa kukusindikiza saloon wanakuwaga kula kulala

    ReplyDelete

Top Post Ad