HII KALI:MAFURIKO YA MOROGORO YASOMBA MPAKA MAJADALA YA KESI MAHAKAMANI

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Magole. Wakati Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Mwanzo Magole, Fredy Mbogela akisema kesi zote zilizokuwa zikisikilizwa katika mahakama hiyo ambayo imesombwa na maji pamoja na mafaili yote, zitaanza upya, Mkuu wa Wilaya na Mkoa wa Morogoro wanahaha kukusanya takwimu za waathirika wa mafuriko.

Mafuriko makubwa yalitokea katikati ya wiki iliyopita Kijiji cha Magole, huku yakisababisha uharibifu mkubwa wa mali na miundombinu. Pia, mafuriko hayo yalisomba majalada ya kesi mbalimbali mahakamani hapo.

Akizungumza jana, Hakimu Mbogela alisema hivi sasa kesi zote za jinai zilizokuwa zikisikilizwa mahakamani hapo zitafunguliwa na kusomwa na kusikilizwa upya.

“Polisi ndiyo watakaofungua na kuzipeleka kesi hizo katika mahakama hiyo, kwa sababu wao wanazo kumbukumbu za kesi hizo kupitia kwa waendesha mashtaka na wapelelezi,” alisema Hakimu Mbogela na kuongeza:

“Hakuna kesi itakayofutwa kutokana kuharibiwa majalada hayo, kama nilivyosema polisi watazileta kesi mahakamani, hata kama kulikuwa na kesi iliyokuwa imekaribia hukumu itaanza upya.” alisema.

Alisema: mahakama itaanza kufanya kazi baada ya kufanyiwa usafi na kuweka samani.

Alisema hatua ya awali ambayo inaendelea kufanywa, ni kusafisha jengo la mahakama hiyo ndani na nje kwa kutoa matope, magogo ya miti na taka nyingine ambazo zilikwama eneo hilo na kwamba, utaratibu wa utendaji unaendelea kufanywa.

Naye Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, Nestory Munjunangoma alisema Idara ya Mahakama kwa kushirikina na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wapo kwenye mchakato wa ukaguzi na tathmini ya uharibifu wa jengo la mahakama hiyo.

Munjunangoma alisema hivi sasa jitihada za kufanya ukaguzi na upembuzi yakinifu zinafanyika kabla ya TBA kutoa ushauri kulingana na uharibifu uliotokea kamajengo hilo linaweza kukarabatiwa ama kujengwa upya.

Alisema hivi sasa shughuli za mahakama hiyo zimesimama, kuruhusu usafi wa mazingira.
Mwananchi
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad