WEMA,DIAMOND WAFUNGIWA KAZI!, MAMA WEMA AWASAKA MTAA KWA MTAA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

HABARI mpya! Mama wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu anadaiwa kuingia rasmi mitaani akiwasaka wapenzi, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Wema, chanzo cha uhakika kimesema na Amani.
Kwa mujibu wa chanzo hicho makini, mama Wema ameamua kuchukua uamuzi huo baada ya kusikia taarifa kutoka kwa watu kwamba, Diamond amekuwa akisambaza maneno mitaani kuwa haogopi vitisho vya mwanamke huyo kufuatia hatua yake ya kumrudia binti yake.
ILIKUWAJE KWANI?
Hivi karibuni, mama Wema alizungumza na gazeti tumbo moja la hili, Ijumaa Wikienda linalotolewa na Kampuni ya Global Publishers Ltd kila siku ya Jumatatu na kusema kitendo cha Diamond kumrudia bintiye hakubaliani nacho.
Aliongeza kuwa, kufuatia hatua hiyo iko siku ataingia mtaani kumsaka Diamond na popote pale atakapomnasa, atamkata na panga.

TURUDI KWA CHANZO
“Jamani si mnakumbuka juzikati mama Wema alisema atamsaka Diamond? Sasa amesikia Diamond anatangaza mitaani kwamba, hatishiki na tamko la mama mkwe wake huyo na watakapokutana watajua nani zaidi.
“Hivi ninavyosema, mama Wema ameingia mtaani kuwasaka. Lengo lake awakute wote wawili ili awaanzishie timbwili la kufa mtu.
“Tangu Ijumaa iliyopita, kila siku anatoka kwenda mitaani kuwasaka, naamini siku akiwakuta pamoja kweli itakuwa vita kubwa,” kilisema chanzo chetu.

KWA NINI ASIENDE NYUMBANI?
Chanzo kilipoulizwa kama kweli mama Wema amepania kuwanasa wawili hao, kwa nini asiwafuate nyumbani kwa binti yake, Kijitonyama, Dar ambako wanapika na kupakua, kilijibu:
“Ameweka mtego wake pale, bahati mbaya sana Diamond naye anaishi kwa machale. Kuna siku anakwenda kulala kuna siku haendi. Huenda na yeye (Diamond) ameweka watu wake ndani kwa Wema wa kumpelelezea kama mama Wema atakwenda au ana dalili za kwenda.”
Chanzo kikaendelea: “Siku hizi Diamond anaweza kwenda kwa Wema, akaacha gari lake na kutoka na la Wema na kurudi kwake usiku sana.”

AMANI LAWASAKA WAHUSIKA
Baada ya kuzinyaka nyeti hizo, Amani liliamua kuutafuta ukweli ambapo Jumanne iliyopita lilimsaka mama Wema kwa njia ya simu lakini iliita bila kupokelewa. 
Amani lilitumia simu zake mbili kumpigia mwanamke huyo.
Baada ya dakika tano, mama huyo mwenye ‘machungu’ na mwanaume yeyote anayemchezea bintiye alituma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) akisema: Nipo msibani tuma sms. Pia akatuma sms kwenye simu ya pili akisema: Nipo msibani, ulikuwa unasemaje?
Amani lilimtumia madai yote kuhusu yeye kuanza kuwatafuta Wema na Diamond, pia likamjulisha kwamba kama anawatafuta kweli, muda huo, wawili hao walikuwa wapo chumbani kwa Wema hawajaamka.
Hata hivyo, mama Wema hakujibu meseji yoyote kati ya hizo mbili hali iliyotafsiriwa na Amani kuwa, uchungu wa msiba ulimuondolea uwezo wa mawasiliano.

NYUMBANI KWA DIAMOND
Mapaparazi wetu walitia timu nyumbani kwa Diamond, Sinza-Mori na kukutana na mtu mmoja aliyedai ni mjomba wa staa huyo ambaye alidai Diamond Platnumz alitoka asubuhi na mama yake, Sanura Kassim kwenda Tegeta, Dar.
NYUMBANI KWA WEMA
Baada ya kutoka nyumbani kwa Diamond huku wakiamini Mbongo Fleva huyo kaenda Tegeta kama alivyosema mjomba mtu, mapaparazi walikwenda nyumbani kwa Wema.
Baada ya kugonga geti kwa dakika moja, alitokea mlinzi na mambo yalikuwa kama ifuatavyo; 
Paparazi: Mambo?

Mlinzi: Poa, karibu.
Paparazi: Asante, nina shida na Wema, sijui nimemkuta?
Mlinzi: Wamelala, hawawezi kuamka muda huu.
Paparazi: Wamelala? Nani na nani?
Mlinzi: Madam (Wema) na Diamond.

Paparazi: Ina maana Diamond yumo ndani?
Mlinzi: Si nimekwambia wamelala?
Paparazi wetu alifanikiwa kupenyeza macho kwenye nafasi ya uzio na kuyaona magari ya wote wawili, la Diamond aina ya Toyota Land Cruiser V8 na la Wema, Toyota Lexus Harrier.
Imeandikwa na Musa Mateja na Shakoor Jongo

GPL
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

19 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Huyo mama hana kaz za kufanya kwa kwel.....

    ReplyDelete
  2. Mmmmmhhhh!! Mama mapenzi hayaingiliwi!! Upo hapo.

    ReplyDelete
  3. mama wema kama huna kazi katafute shamba ulime mihogo kuliko kuwashulikia hao na mambo
    yao! wema ingelikuwa ni mtoto hapo ningekubaliana nawe!

    ReplyDelete
  4. Wacha mucous iendeleee mama wema mkorofi sana sana

    ReplyDelete
  5. Hv we mama bdo unalichunga hilo gume gume??

    ReplyDelete
    Replies
    1. wewe ndo unaona ligume gume ila yeye anaona binte yake mpendwa wa pekee

      Delete
  6. Mama wema atulie ama anataka huyo binti yake amtafutie yeye bwana? Aaaahhh makubwa haya sasa atamharibia mwanaye asipochunga huyu mama. Ama anaona raha akisikika kwenye magazeti naye? Ela napita yangu macho kazi ni kuangalia.

    ReplyDelete
  7. Huyo mama kavurugwa anitafute nimtibu.

    ReplyDelete
  8. Mama acha kujiaibisha aise

    ReplyDelete
  9. mama wema acha movie iendelee

    ReplyDelete
  10. jamani mama achawatoto damuzimeendana achakumzalilisha mwanao huwezijua keshoitakuwaje diamond akawamsaidizi wako umezeka ukaendakwao leounawazalilisha hivyo watakiebaraka wanaowaishi kwaamani.

    ReplyDelete
  11. thanks guys for your good udaku news

    ReplyDelete
  12. Uyo mama vp?mbona ivo kwan wema ni mtoto ad amchunge?

    ReplyDelete
  13. Jamani mama wema huna kazi ya kufanya.vijana wanapendana acha kumdhalilisha binti yako

    ReplyDelete
  14. Hakuna lolote mtu mzima awezi kufanya kazi ya kijinga kama hiyo ila nn nyie watu wa mitandao ndiyo waongo sana na ndiyo hamna kazi kufatilia maisha ya watu si mtoe zeni za mitaani huko mbona amusemi zenu tulieni andikeni vitu va mana na akili siyo muna kurupuka tuu sijui wawapi nyie watu

    ReplyDelete
  15. Huyu mamatumemchoka yeye na mwanae warudi unyaturuni kwao khaa kwa wema gani basi domo kama......

    ReplyDelete
  16. Wema ni malaya pori

    ReplyDelete
  17. na mama yako yeye ni malaya msitu au ↑

    ReplyDelete

Top Post Ad