AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wakaazi wa kijiji kimoja huko Magharibi mwa Sri Lanka wamekutwa na neema ya aina yake baada ya kunyeshewa mvua ya samaki wadogo wanaofaa kwa kitoweo.
Wakielezea tukio hilo, wanakijiji hao wamesema walisikia kitu kizito kikidondoka waligundua kuwa ni samaki, waliwakinga samaki hao na waliwapata wengi wenye uzani wa kilo hamsini ambao waliweza kuwatumia kama kitoweo.
Kwa mujibu wa BBC, Wanasayansi wameeleza kuwa mvua ya samaki hutokea wakati ambapo upepo mkali unakuwa juu ya maji ya kina kifupi na kusababisha mzunguko wa maji unaovuta karibu kila kitu kilicho ndani ya maji ikiwa ni pamoja na samaki na vyura.
Wameeleza kuwa viumbe hao wa majini wanaweza wakasafirishwa kwa masafa marefu na kushikiliwa na mawingu kwa muda hata baada ya ule mzunguko wa maji kuisha, na baadae wanashuka kama mvua.
Tukio la aina hii liliwahi kutokea Sri Lanka mwaka 2012 ambapo mvua ya samaki aina ya kamba wa baharini ilinyesha kwa mtindo huo.
Mvua hii ikinyesha vijijini huenda wanakijiji wakaomba iwe ya mafuriko ya samaki…anyways, ingekuwa vipi kama mvua inayonyesha sasa hivi Dar es Salaam ingekuwa mvua ya samaki wanaotumika kwa kitoweo?
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Ivi mitandao yakijamii uongo mumezoeya
ReplyDelete