AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Peraira Silima, alisema tabia hiyo ya trafiki ni kinyume cha sheria na zinaweza kusababisha ajali.
Hata hivyo, Silima aliwataka madereva kutii Sheria za Barabarani ikiwemo kupunguza mwendokasi na kufafanua kuwa, wakati mwingine askari hutafuta kivuli na hatua hiyo isichukuliwe kuwa wanavizia magari.
Katika swali lake, Ngoye alitaka Serikali ieleze ni hatua gani zimekuwa zikichukuliwa kuhakikisha madereva wanafuata sheria zilizowekwa kama inavyofanyika katika nchi nyingine.
Ngoye pia alitaka Serikali ieleze kwa nini madereva wameendelea kutumia magogo, mawe na majani yenye miba barabarani kuashiria kuwa kuna gari limeharibika, na wakiondoka wanayaacha na wengine wameendelea kuendesha magari huku wakisikiliza simu.
Naye Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema), alihoji kama ni sahihi kwa trafiki kuvizia magari na kifaa cha kupima mwendo kasi.
Akifafanua majibu ya maswali hayo, Silima alisema trafiki kujificha na chombo hicho na kujitokeza kusimamisha gari ni kinyume cha sheria kwa kuwa tabia hiyo inaweza kusababisha ajali.
Kuhusu matumizi ya magogo, majani na mawe, alisema ni kinyume na Sheria na kutaka madereva watumie alama za pembe tatu ambazo ni nzito na kuachana na alama hizo ambazo ni nyepesi ambazo hupeperushwa na upepo.
Silima pia alionya kuwa Serikali iko mbioni kuanza kuwanyang’anya leseni za udereva madereva wote ambao watathibitika kukithiri kwa makosa ya usalama barabarani, na kuzuiwa kabisa kufanya kazi hiyo.
Hatua hiyo itaanza kuchukuliwa mara baada ya kukamilika na kuanza kwa Mfumo mpya wa Nukta, ambao utaweka kumbukumbu za makosa ya madereva ambayo itatumika kuwachukulia hatua hiyo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
yah ni kweli lakini muwatafutie vizuia mvua na jua
ReplyDeleteHawaba lolote wanataka rushwa tu
ReplyDeleteKaz dawa
ReplyDelete