Mtuhumiwa Amng’ata Mdomo Askari

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

KARANI wa Kampuni ya Mabasi ya abiria yaitwayo Happy African, Eliud Mwanyonga (40), amemng’ata mdomo askari wa kikundi cha ulinzi shirikishi aliyefahamika kwa jina moja la Ernest.

Tukio hilo lilitokea Ijumaa iliyopita saa 12 alfajiri katika Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani wakati askari huyo alipokuwa katika shughuli zake za kila siku.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, James Zebedayo, aliliambia MTANZANIA Jumatatu kwamba, askari huyo aling’atwa mdomo baada ya kutaka kumkamata Eliud kwa kosa la 
kutovaa sare za kazi.

“Hawa mgambo walikuja asubuhi walikuwa kama sita hivi na walipofika hapa wakawa wamemuuliza kwanini hakuwa na sare.

“Yeye akawajibu siku hiyo ilikuwa ni Siku ya Mashujaa, kwa hiyo hakuwa na sababu ya kuvaa sare.

“Alipojibu hivyo yule askari wakachachamaa, wakasema lazima amkamate ili akaadhibiwe kisheria lakini yule mfanyakazi akakataa akasema hawezi kukamatwa mara mbili kwa kuwa alikuwa amekamatwa siku chache zilizopita kwa kosa lile lile.

“Baadaye huyo mtuhumiwa alifanikiwa kuwakimbia lakini askari hao walimkimbiza na walipomkamata, walimpiga kwa kutumia fimbo walizokuwa nazo. Walipokuwa wakimpiga, mtuhumiwa naye alijitetea na mwishowe akamng’ata askari huyo mdomo wa chini na kuuondoa kabisa,” alisema Zebedayo.

Kutokana na tukio hilo, askari wengine walifanikiwa kumdhibti mtuhumiwa huyo na kumpeleka katika Kituo cha Polisi kilichoko kituoni hapo kabla ya kupelekwa Kituo cha Polisi Magomeni ambako alifunguliwa jalada lenye namba MAG/RB/7172/2014.

Naye Mkuu wa Kituo cha Polisi Ubungo, Suphiani Masanga, alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo ingawa hakutaka kulizungumzia zaidi kwa alichosema kuwa yeye siyo msemaji wa Jeshi la Polisi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad