AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Samatta amekuwa akidaiwa kunyemelewa na baadhi ya timu kutoka mataifa ya Ulaya kama vile Ufaransa, Ureno, Urusi na Ubelgiji, kutokana na kipaji kikubwa anachokionyesha cha kusakata kabumbu.
Samatta aliliambia Udaku kwa njia ya mtandao kutoka nchini Tunisia ilipoweka kambi Mazembe kuwa ndani ya miaka miwili ijayo amepanga kucheza soka kwenye ligi kubwa barani Ulaya na tayari ameshazungumza na Katumbi juu ya suala hilo na amekubaliana naye.
“Nimepanga ndani ya miaka miwili ijayo nicheze kwenye ligi kubwa ulimwenguni, nimezungumza na bosi wa timu, Katumbi kaniruhusu na kuniambia suala hilo halina tatizo, pia amesema ataniachia na hawatanibania timu ikija kunisajili,” alisema Samatta.
Katika hatua nyingine, Samatta alisema timu yao imeshindwa kuweka kambi barani Ulaya kwenye nchi ya Ubelgiji kutokana na baadhi ya wachezaji kukosa viza ya kuingilia nchini humo. Kwa sasa wapo nchini Tunisia wakijiandaa na mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Zamalek ya Misri.
Kwa miaka mingi sasa Mazembe imekuwa ikidaiwa kuwabania nyota wake kujiunga na timu za Ulaya kwa lengo la kujiimarisha, lakini msimu uliopita ilimuuza nahodha wake, Tresor Mputu, kwenda timu ya Kabuscorp ya Angola aliyokuwa akichezea Mbrazil, Rivaldo,
Mazembe pia imemuuza beki raia wa Zambia, Stopilla Sunzu, aliyesajiliwa na Sochaux ya Ufaransa inayonolewa na kocha wa zamani wa Zambia, Herve Renard.
Samatta alijiunga na Mazembe mwaka 2011 akitokea timu ya Simba, iliyomuuza kwa dau la Dola za Kimarekani 100,000 (sawa na Sh. milioni 150 za Tanzania za wakati huo), huku yeye mwenyewe akipewa Dola za Kimarekani 50,000 za usajili.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
amechelewa umri umeshakwenda
ReplyDeleteunatombwa ww mdau hapo juu umli umekwenda kwani samatha ana miaka mingap? sio unaongea2 kama una kipisi cha mboo matakon
ReplyDeleteuyo mdau wa apo juu msenge kjana umr bado unadai na soka analweza we unafkr n anko ngassa uyo alielzka kumalzia soka ake bongo ksa tu acheze yanga watu wanaangalia mbel co cmba na yanga tu
ReplyDelete