Chid Benz Zingatia Haya ili Usirudi Ulipotoka La Sivyo Tutakupoteza Kama Wengine

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kati ya watu ambao hawakufiri kama msaanii Chid benz angeweza kurudi vyema kwenye ulingo wa muziki Mimi ni mmoja wapo maana nilihisi kama huyu mtu amesha changanyikiwa na amepoteza uwezo wa kufikiri au kukaa chini akatunga wimbo mzuri tena.

Pengine mwenendo wake na tabia zake zilimponza na sasa amejua pakurekebisha. Chid Benz ni kati ya wasanii waliopendwa na wengi na alipata mafanikio makubwa kupitia mziki wake na akabweteka na kujisahau!

Ujio wake mpya umenifurahisha sana na hakika tunaanza kumuona Chid Benz yule wa wimbo kama" Dares-salaam stand up" na nimefarijika sana kumsikia karudi rasmi na huyu ndio Chid benz ambaye tumekuwa tukimfahamu.

Wanajamvi hasa wale wapenzi wa burudani kama mmepata nafasi ya kuusikiliza wimbo wake unaoitwa "Mpaka kuchee" ambao amewashirikisha Diamond na Ay mtakubaliana nami kuwa huyu ndio Chid Benz mwenyewe maana mule ka rapu vyema naona sasa yuko serious!

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni ...Diamond anajua kutumia nafasi anazopewa hasa kwenye kuimba, kwakweli kwenye wimbo huu kaimba vizuri sana na kautendea haki wimbo huu!Hata Ay mzee wa biashara ametenda haki nusu afunike.... kwakweli walijipanga big up sana kwa zawadi hii.

USHAURI KWA CHID BENZ

Kuna mambo ambayo amekuwa akifanya Chid benz na huwa kera wengi hasa sisi mashabiki wake mfano ...Kupigana hovyo,Kupiga hovyo,Matumizi ya madawa na bangi
hayo inabidi aachane nayo maana yanamchango mkubwa kuharibu muziki na kipaji chake.

Hawa alio imba nao ndio wanaweza kuwa muongozo wake hasa Ay anaweza akamsaidia sana kama akiamua kuwa sambamba nae.
Nivyema akaangalia aina ya marafiki ambao amekuwa nao siku zote ambao wamempelekea kuzama kwenye madawa inabidi awapunguze na afanye muziki sasa.

Namtakia kila la kheri kwenye safari alio ianza upya.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. bangi nibangue nitunge mistari mitamu, sijui ni aina ipi ya foolish age wanayopitia wenzetu jamani, Chidi wewe ni mkali Sana ni kweli Mimi kama shabiki nimeanza kuona sala za mashabiki zinafanya kazi bado Mungu anakupenda dogo pambana achana na cerelac, tena tutafurahi ukimshauri na mnyama

    ReplyDelete

Top Post Ad