AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mama Tibaijuka, hivi kweli anaweza kusimama mbele ya umma na kusema pesa alizopewa sio chafu? Hivi ni kweli alipokuwa UN aliwahi kupokea pesa za namna hiyo? Sasa kwa nini anakuja kupokea akiwa Waziri wa CCM? Askofu Kilaini hata na yeye naye anaweza kweli kukubali kupokea Shillingi Millioni 80 bila ya kuzifanyia kazi inawezekana vipi? Hizi pesa walipewa za Rushwa nia na madhumuni ilikuwa kuwanunua their influence, wamekamatwa red handed tunapoteza muda kujadili bungeni kujadili nini na ukweli upo wazi kuwa wamepewa pesa na wamezipokea!
- Kwanza warudishe hizo pesa kwa waliowapa, and then hatua za kinidhamu zichukuliwe na hasa kutoka kwa Chama cha Mapinduzi, wale wote walio wanachama wa CCM waliopokea hizo pesa chafu wachukuliwe hatua na ikibidi waende Mahakamani kwa kupokea Rushwa, huyo Askofu watajijua wenyewe huko Kanisani kwake ila I hope hatahubiri tena ila ndio maana sijawahi hata kumsikiliza nilishamshitukia siku nyingi kuwa hayupo kwenye mstari na Mungu, wanajifanya kupiga piga kelele za siasa kumbe wanatafuta mlo tu na hizi siasa za kuwachanganya Maaskofu sijui tumezianza lini Tanzania.
- Warudishe Pesa chafu ni za Rushwa na halafu waadhibiwe na CCM and then Sheria ichukue mkondo wake si kuna Rushwa hapo!!
Le Mutuz
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK