Pinda, Werema na Muhongo wataka zigo la Escrow abebeshwe Kikwete!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Dodoma kumekucha. Naomba kwa ufupi niwafahamishe kinachojiri maeneo haya (nimepiga kambi huku).

MOSI:
Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa anataka PM Pinda atoke kwa sababu mbili, moja ili njia ya kupata Urais iwe nyeupe lakini pili ili asiwe PM peke yake aliyewahi kujiuzulu kwa tuhuma za rushwa. Watu wake Edward wanahangaika sana kushawishi watu ili azma hii itimie.

PILI:
Membe naye anataka PM ang'oke kwa sababu kuu mbili, moja ili njia ya Urais iwe rahisi lakini pia kwa matumaini kwamba anaweza kupata yeye uPM japo kwa muda tu ili nyota ing'are zaidi.

TATU:
Wassira naye anatakaPinda aanguke ili njia iwe rahisi lakini pia kwa matumaini kwamba anaweza kupata yeye uPM.
Mwandosya naye anataka PM adondoke kwa matumaini ya kupata uPM kutokana na utu uzima.

Sitta naye vivyo hivyo.

NNE:
Mawaziri walioondolewa huko nyuma wakiongozwa na Kagasheki, Nchimbi na Maige nao wanaomba Serikali idondoke kwa sababu wanaamini Pinda aliwatosa ili apone yeye na sasa wanataka na yeye awajibike kwa udhaifu wake. Yupo mtu kama Mwigulu ambaye anautaka Uwaziri kamili kwa udi na uvumba na anataka Serikali ianguke ili Baraza la Mawaziri lisukwe upya awe Waziri kamili.

Kambi za Urais za wazee zimeungana kutaka Pinda ang'oke!

TANO:
Kwa upande mwingine hii ni vita ya watu wa Mara: Maswi, Muhongo, Werema na Mkono. 

Upande mwingine ni vita ya baina ya vizazi; kizazi cha vijana na kizazi cha wazee.

Tazama Vijana walioshikilia bango suala hili ni wabunge vijana: Zitto, Kafulila, Filikunjombe, Serukamba, Mpina, Bulaya, Kigwangalla n.k.

Wanaotetea ni watu wazima: Pinda, Muhongo, Werema na wengine.

Lakini pia kwa Upande mwingine ni vita ya pesa: Kila upande umekula na ujanja ni kuwahi kupaka matope wengine!

SITA:
Kamati ya PAC imeandika ripoti nzito zaidi ya ripoti ya CAG ambayo ni laini mno (nimebahatika kuziona walau zote mbili). PAC, chini ya Zitto na Filikunjombe wanaweza kuwa wamefanikisha kufanya ripoti yao iwe vizuri hivyo kwa sababu wamewahoji watu na kupata taarifa za ziada (ambazo zitaibua mjadala mzito sana Bungeni).

SABA:
Pinda anapigana kufa na kupona ili apone. Pinda akianguka hapa Urais ndio kwisha. Hata hivyo, Pinda hata asipotoka uPM atakuwa tayari amechafuka na udhaifu wake umebainika. Ijapokuwa Wabunge wanaweza kumponya tu Pinda kwa sababu ya kumsaidia Kikwete lakini tayari ana doa!

Hata hivyo, katika harakati za kupona Pinda, Werema na Muhongo wamekuwa wanawaambia wabunge kwamba kulikuwa na agizo la Rais la pesa kulipwa. Yaani Pinda yuko tayari kumuingiza Rais kwenye tope kulinda vyeo vyao!

Kikwete inabidi afanye maamuzi ya Kiurais, watu aliowaamini hawana hiyana kumtosa. Akimaliza Urais ndio hatari zaidi (mtakumbuka kauli yangu 2016/2017)
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad