AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili hivi karibuni, waziri huyo alisema kuwa itakuwa ni kosa iwapo Rais Jakaya Kikwete atakabidhi kijiti kwa mtu mwenye umri unaofanana naye.
Nyalandu alibainisha kwamba wakati ukifika, atatangaza iwapo atagombea urais au kuendelea kugombea ubunge katika jimbo lake la Singida Kaskazini.
“Ukifika wakati ni lazima kubadilishana vijiti. Ni lazima kizazi kinachomaliza muda wake, kikabidhi kijiti kwa kizazi kinachofuata. Ni wazi mtu mwenye umri unaofanana na kiongozi anayeondoka madarakani hana nafasi,” alisema Nyalandu akiongeza:
“Kijiti hiki anachokiacha Jakaya Kikwete, aliachiwa na kaka yake Rais Benjamin Mkapa na Mkapa naye aliachiwa kijiti na kaka yake Mzee Ali Hassan Mwinyi ambaye ndiye alisema kila zama na kitabu chake.”
Alieleza kuwa huo ni uhalisia wa maisha na kwamba ni lazima kila mtu kukubali hivyo.
“Sasa tunahangaika kuandika hitimisho la zama za Rais Kikwete, ndiyo sisi tunapambana kuhakikisha tunakomesha ujangili na wengine wanafanya kazi nyingine. Haya yakikamilika ni zama zake (Rais Kikwete), zimekamilika,” alisema Nyalandu.
Alifafanua: “Rais Kikwete atakabidhi kitabu kwa zama nyingine na sharti akabidhi kijiti kwa kizazi kinachofuata. Haitawezekana ikiwa atakabidhi kijiti kwa kizazi chake hichohicho. Ni kosa kurudia zama zilizopita.”
Nyalandu alisema kuwa ni vyema mtu yeyote mwenye umri unaofanana na kiongozi anayeondoka madarakani akasahau kupewa kijiti kwani historia na hata maandiko ya Mungu vipo tofauti.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
MICHOSHOO KUTWA KUWAZA UFISADI NA MUFILISI WA HILI TAIFA
ReplyDeletehivi huuu uraisi ni kwamba unachaguliwa na watuuu? au unajiamulia mwenyewe? haya majamaaa vipi? nani kamwambia huyu jamaa afikirie anachokisema?
ReplyDeletehao vijana wanaopiga wazee jamani itakua nchi au balaa kwakweli urais unatakiwa hekima na ujasiri wa hali ya juu kwani vijana wa hapa kwetu bado kufikia kuwa rais kwani wana jaziba siszo kuwa na maana na sitarehe nyingi
ReplyDeletevijana hawa wapumbavu kabisa, hamna kitu hapo, c unaona wanapiga mpaka baba zao.
ReplyDelete