AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
(Jina Langu) samahani, nikamjibu...bila samahani...(Jina lake), nina shida ya sh.30,000/= naomba unisaidie,(kwa kuwa nimezoena nae sana akaanza kunisimulia)
Kuna hawara yake ni doctor hapa ...juzi yake alimwambia kuwa "hamtaki tena kuanzia Juzi hiyo" huyo hawara yake ana mke na watoto 3.
Ni yeye (hawara) ndiye anayemlipia kodi ya nyumba, anamsomesha chuo cha Hotel management na ndiye anayemtunza kwa maana ya chakula.
Sasa kodi inaisha mwezi wa kwanza mwakani na ada ya chuo anadaiwa na imebaki sh. 700,000/= na pesa ya kwendea field Zanzibar hana.
Akaniambia kuwa, ...Nimepata mtaalamu (mganga) ameniambia nimpe sh. 30,000/= ili anipe dawa nimvute, (Amchomee) ili kurudisha mawasiliano halafu nyingine atamwekea kwenye chakula au kinywaji ili "akiomba kiasi chochote kile cha pesa apewe"
Sikuwa na iyana ila nimuuliza swali moja, kwa nini usitumie njia ya mazungumzo? akasema nishajaribu sana but hataki! "sasa mimi nitaishije hapa wakati ada nadaiwa, kodi ya nyumba inaisha mwakani"?
Nilimpa sh. 30,000/= akaenda.
Jumapili (jana) huyo hawara yake alisalimu amri yy mwenyewe kwa yeye kuanza kumpigia simu (kwa mujibu wa huyu binti) jamaa alimuuliza "upo wapi"? demu akajibu nipo nyumbani, Njoo .....bar...sasa kilichojiri huko jana sikijui nadhani leo ataniambia tu..
Kwa hiyo, wanaume tuwe makini sana na mahawara kwani yawezekana unaye na unatamani ujinasue kwake ila moyo wako unakufa ghafla na kuamua kuendelea naye hadi sasa. Pls, tuwe makini sana.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Hapo ukishanasa ndio umenasa, ndumba hazina umakini, labda atokee mtu mwingine/nduguyo ashtuke akuokoe ndio itakuwa salama yako, vinginevyo na mkeo utamwacha utangaze ndoa na hawara. Lakini mengine wanaume mnayataka wenyewe, kila siku mnaambiwa michepuko sio dili hamsikii, wacha yawakute!
ReplyDelete