Stara Thomas Awaponda Wasanii na Maproducer wa Bongo Flava

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msanii wa muziki Stara Thomas amefunguka kwa kusema kuwa wasanii wanashindwa kufika mbali kutokana na uoga na kutokuwa serious na kazi zao.

Stara ameiambia Bongo5 kuwa wasanii wa sasa wanashindwa kujitanua zaidi.

“Asilimia kubwa ya wasanii waoga, bado wamekuwa na akili za kujiangalia hapa walipo, wengi bado hawajapata akili ya kutoka na kujitegemea wenyewe nje, hii inawafanya wasanii wengi wasikue wabaki pale pale,” alisema Stara.

Pia Stara alisema watayarishaji wa muziki wanachangia kuuangusha muziki kutokana na kushindwa kuwa wabunifu.

“Wapo maproduce wazuri lakini njia wanazo zitumia zinafanya muziki unafanana, wengi wanakuwa wanaandika juu wa beat tofauti na zamani sisi tunaandika kwanza ndo beat inatengenezwa, kwahiyo unakuta anayeandika anakuwa controlled na beat, kwahiyo kama producer alitengeneza beat inafanana katika watu watatu au wanne basi hata kile kinachokuja kuimbwa kitapenya katika ile melody,” alisema Stara.

Pia Stara ameongeza kuwa sasa amerudi rasmi kwenye muziki huku akiwataka mashabiki wa muziki wake kuendelea kusupport kazi zake.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad