AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Staa huyo aliwahi kukiri kuwa na uhusiano huo na msanii huyo na kwamba walishaachana kwa amani, ndiyo maana waliweza kuendelea na kampuni yao ya masuala ya filamu ya Rj Company.
Juzi Johari ameliambia gazeti la Mtanzania kwamba, muda mrefu alikuwa akisikiliza wanaodai hana uelewano mzuri na Ray kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji Chuchu Hans na sasa ameamua kuweka wazi suala hilo.
“Ni kwa kipindi kirefu sana yamezuka maneno yanayodai mimi na Ray tulishawahi kuwa wapenzi, kitu ambacho si cha kweli, tena kibaya zaidi wameongeza kuwa hatuna maelewano mazuri kikazi,” alieleza Johari.
Aliendelea kufafanua: “Sikuwahi kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi kama wengi wanavyofikiria na kama ningekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Ray na tumeachana, hata kampuni yetu ingeshavunjika kwa kuwa tungekuwa na chuki, nawaambia hatutegemei kutengana kikazi wala kirafiki,” alisema Johari
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK