TETESI za Kutoweka Kwa Jack Cliff Gerezani Huko China..Serekali yapaswa Kulitolea Ufafanuzi Hii Habari

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jana Katika Mitandao Mbali mbali zimeenea taarifa ambazo bado hazijafahamika kama ni za kweli ama la kuwa Mtanzania Mwenzetu Jack Cliff Aliyekamatwa kwa Madawa ya kulevya Nchini China ametoweka Gerezani na kupelekwa kusikojulikana....

Habari inayozunguka mitandaoni ni hii hapa:


  • Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya China vimeriport kuwa Mtanzania aliekuwa anazuiliwa katika gereza moja huko China ametoweka na kuperekwa kusikojulikana. Habari zinasema mtanzania huyo alikuwa anasubiri hukumu ya kifo kufuatia kukamatwa na madawa kulevya.


Tunaomba serikali itolee ufafanuzi Habari hii au kama kashatekelezewa hukumu yake, pia tujue! Lazima government yetu ithamini raia wake hata kama wana makosa
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

9 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. WACHINA WAMESHA WACHOKA HAWA WA MADAWA YA KUREVYA SASA, WAKITANGAZA, WANAMBIWA WANAVUNJA HKI ZA BINADAMU, SASA ILIYOBAKI WANACHUKUA TU MAMUZI YAO KWA KUFWATA SHERIA ZAO BILA KUWATANGAZIA. NDIO MUACHE KUWAPELEKEA MIDAWA YA KUREVYA, MMJIARIBU WENYEWE HUKO HUKO KWETU, WAO WANAVYFWATA SHERIA ZAO, NA HAKUNA BLABLA

    ReplyDelete
  2. Duh!Mdau wa hapo juu wakati somo la kiswahili likifundishwa ulikuwa unalala nini darasani? Una tatizo la kujua wapi uweke herufi ya "L"au "R" Labda umetokea katika upande wa ziwa magharibi nini?

    ReplyDelete
  3. Heheheh umemuona huyo tuu? Je na alie andika tarifa/udaku je? KUWEKWA hiiii ni shidaaaaaaa

    ReplyDelete
  4. Na wewe unae jaribu kumtetea huyo mwenzako hapo juu pia umechemsha(ni taarifa na sio "tarifa")Au ndio wale wale kiswahili ni lugha yetu lakini bado ni kigumu sana kati yetu sisi wabongo walijisemeaga Wazaramo"ZILONGWA MBALI NA ZITENDWAZO MBALI"Upo hapo

    ReplyDelete
  5. Anonymous wa kwanza lazima atakuwa mkurya.

    ReplyDelete
  6. ati kuperekwa! alafu wewe unamiliki mtandao wa kijamii, duu! Tz bado sana. alafu anaemkosoa mwenzake anasema magharibi, duuh! ama unamaanisha ziwa tanganyika?
    hebu hata kuandika tuwe makini basi, admin anakosea na wadau pia

    ReplyDelete
  7. Duh kiswahili kweli ni lugha ngumu sana mdau wa hapo umeandika neno "alafu badala ya "halafu" unamkosoa mwenzako wakati wewe mwenyewe sentensi zako pia hazijakamilika kuweni makini mnapoandika maoni yenu kabla ya kuya send rudieni kuyasoma tena yale mliyo yaandika ili kama kuna makosa muya sahihishe msituharibie lugha yetu nzuri

    ReplyDelete
  8. kiswahli kilikuja na meli jamani

    ReplyDelete

Top Post Ad