Fedha alizochangiwa Lowassa na kundi la Marafiki wa Edward Lowassa zatafunwa....

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Na Makongoro Oging’
WANACHAMA wa kundi la Marafiki wa Edward Lowassa waliochanga fedha za kumwezesha waziri mkuu huyo wa zamani kuchukua fomu ya kugombea urais, wamemtuhumu aliyekuwa naibu katibu wao, George Kivuyo  kutafuna fedha hizo.
Taarifa zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya wanachama hao wanaojulikana kama Team Lowassa 4 President, zinadai naibu katibu mkuu huyo ambaye pia ni mweka hazina wao, alitafuna kiasi cha shilingi laki saba zilizochangwa.
Walidai fedha hizo ziligunduliwa kutotumika ilivyopaswa baada ya kutojulikana zilipo na alipoulizwa hakuwa na majibu ya kueleweka.
Baadhi ya wanachama hao, Fauzia Ally, Hassan Mollel na Yussuf Hamis walisema kutokana na kitendo hicho, wanachama hao wameanza kufarakana kutokana na mgogoro.
“Hizi fedha zilitumiwa tofauti na ilivyokusudiwa, zinatakiwa zirudishwe, akabidhiwe mzee Lowassa,” alisema Hassan Mollel.
Naibu katibu mkuu huyo alipopigiwa simu na mwandishi wetu juzi Jumapili alisema kwamba madai hayo ni ya uongo na fedha hizo hazikuwa laki saba bali zilikuwa Sh. 526,000.
“Mimi ni mweka hazina msaidizi na tatizo limekuja baada ya kuhoji kuhusu fedha hizo alizokabidhiwa bosi wangu.”
Katibu mkuu wa chama hicho, Mohamed Mkindi alipoulizwa alikiri kusikia malalamiko hayo lakini alidai yupo mikoani na akirudi jijini Dar es Salaam atazifuatilia.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad