AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Amesema madai kuwa ataibeba Serikali kwa kuwa ni mbunge wa kuteuliwa hayana msingi kwa kuwa haendi bungeni kumtumikia rais bali kuwatumikia Watanzania.
Rais John Magufuli Jumatatu wiki hii alimteua Dk. Ackson kuwa mbunge wa kuteuliwa na kutengua nafasi yake ya naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali aliyoteuliwa hivi karibuni na Rais mstaafu, Jakaya Kikwete.
“Ni kweli nimeteuliwa na rais, lakini nakwenda kufanya kazi za Watanzania, nikipata nafasi ya kuwa naibu Spika madai kuwa nitaibeba serikali hayapo kwa kuwa nitafanya kazi za Bunge ambazo ni kuisimamia, kuishauri na kuiwajibisha serikali,” alisema Dk. Ackson ambaye juzi usiku alipitishwa kwa kauli moja na wabunge wa CCM kuwa mgombea wake wa unaibu spika.
Alisema ni vyema wabunge wakawa na imani naye na kumpa ushirikiano wa dhati ili atekeleze majukumu yake ipasavyo.
Katika hatua nyingine, vita ya unaibu Spika wa Bunge la 11, imemalizika, baada ya, Dk. Ackson, kupitishwa kwa kauli moja na wabunge wa CCM kugombea nafasi hiyo.
Awali kulikuwa na mvutano wa ndani kwa ndani baina ya wabunge wa chama hicho, ambao waligawanyika kwa baadhi kumtaka Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Kwenda wewe ulivyonda haraka haraka hivi
ReplyDeleteSisi si wajinga hivyo
Haijatoke Tanzania
UTAUMWA SANA, HAKUNA WA KUKUTIBU!!!
DeleteNDO'BASI TENA
ALOPEWA'KAPEWA
Naibu mwanasheria mkuu
ReplyDeleteKwa ajiliM 200
Mara ugombee uspika CCM wakachemsha kwani ulitakiwa uaache unaibu mwanasheria
Mara unajitoa unagombea unaibu spika
Hiiii inashangaza hata kwa maiti
Tena una PhD ya sheria
Shame you CCM
Utapita kwa wingi WA wana CCM lakini ni mkono wa Mtu
Utawakuta bungeni wenye sheria Kama yako wanavyoijua sheria Na kanuni za bunge
Imewauma hiyoooo........imewachoooooma kama pasi..... CCM woyeeeeee!!
DeleteMtakondaje mwaka huu.........MTAISOMA NAMBA
Mtaisoma namba nyiye muishio bongo
DeleteUghaibuni tuna raha zetu
Kama unaona kuwa ugaibuni ndio umefanikiwa kwa nini unahangaika na habari za Tanzania? wewe wala haujielewi, na huko unafanya kazi za kitumwa na utakuwa mtumwa mpaka mwisho maana haujitambui
DeleteLakini hatuibi na mafisadi
DeleteTumechoka kusaidia ndugu zetu kwa ajili ya CCM