AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kingunge |
Akizungumza kwa njia ya simu baada ya kuombwa kutoa maoni yake kuhusu Uchaguzi Mkuu uliomalizika hivi karibuni na Dk John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutangazwa mshindi, Kingunge bila kufafanua zaidi alisema: “Nitazungumzia mchakato wa uchaguzi baadaye baada ya kukamilisha kukusanya taarifa.”
Mwanzoni mwa Oktoba, Kingunge ambaye amekuwa kada wa CCM kwa miaka 61 (tangu enzi za TANU), alitangaza kujitoa katika chama hicho akisema hawezi kuendelea kuwa ndani ya chama kinachoendeshwa kwa maslahi binafsi.
Kingunge ambaye amefanya kazi kwa karibu ndani ya CCM na Serikali na marais wa wote wa awamu nne, alidai chama hicho kimepoteza mwelekeo na hakijadili mambo muhimu kama ilivyokuwa zamani.
Pamoja na Kingunge kudai hajiungi na chama kingine chochote cha siasa, alionekana kwenye jukwaa la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wakati wa kumnadi mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho aliyeungwa na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa.
Uchaguzi Mkuu ulifanyika Oktoba 25, mwaka huu, na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilimtangaza Dk John Magufuli kuwa mshindi baada ya kupata kura 8,882,935 (asilimia 58.46) na kufuatiwa na Lowassa kura 6,072,848 (asilimia 39.97).
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Babu tulia nyumbani usijiletee matatizo kwa mambo ya uchochezi
ReplyDeleteakafie mbele
ReplyDeleteHiki kibabu nj mmoja kati ya wale Magufuli alomwambia JK kwamba alikuwa anafanya kazi na WANAFIKI..........KINGUNGE UMEISHIWA PUMZI, HUNA NGOMA WALA NYIMBO......HEBU TUPISHE TUPITE........... CCM MBELE KWA MBELE
ReplyDeleteNdio imekula kwako tayari,hukueleweka kabla ya uchaguzi ndio itakua leo?
ReplyDeleteMzee unameza matonge kwa picha ya samaki sasa.lol.