Mwanamke Ashambuliwa Kwa Kuzungumza Kiswahili Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwanamke aitwaye, Asma Jama ameshambuliwa nchini Marekani kwa kuongea Kiswahili.

Jama alikuwa amekaa na familia yake kwenye mgahawa wa Applebee huko Minnesota, akikata kiu na juice huku mazungumzo yakiendelea kabla ya kujeruhiwa vibaya mdomoni. Mwanamke aliyekuwa amekaa jirani yake alimponda na glasi nzito ya bia mdomoni.

Sababu? Jama alikuwa akizungumza Kiswahili na familia yake.

Siamini baada ya miaka yote hii mtu ananipiga sababu niko tofauti,” alisema Jama. “Mtu ananipiga kwasababu nilikuwa nikizungumza lugha ya kigeni.”

Shambulio lilimwacha Jama na majeraha usoni pamoja na mdomo kuchanika kiasi cha kushonwa nyuzi 17.

Jodie Burchard-Risch, 43, na mume wake, walikuwa wamekaa kwenye mgahawa huo jirani na Jama, aliyekuwa ameketi na binamu na watoto wa nduguze. Wawili hao walichukizwa baada ya kumsikiliza Jama na familia yake wakizungumza lugha ngeni.



Jama alisema wawili hao waliwaambia waende nyumbani. “Walisema ukiwa Marekani unatakiwa kuzungumza Kiingereza.”

Jama, ambaye ni msomali, alihamia Minnesota mwaka 2000 kutoka Kenya. Anazungumza lugha: Kiingereza, Kiswahili na Kisomali.

Jumatatu hii, Burchard-Risch alishikiliwa kwa kosa la shambulio.

Kutokana na shambulio hilo, Jama anadai hana amani tena na anafikiria kuhama Minnesota. Amesema anaweza kuungana na dada yake aliyehama Minnesota mwezi June na kwenda Dallas.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hawa wazungu hawatupendi na sisi tusiwapende vilevile walitaka wawe pekeyao hapa duniani

    ReplyDelete
  2. Nilidhani anataka kurudi Somalia au Kenya, kumbe bado hataki kuhama ila anazunguka humo humo

    ReplyDelete
  3. wakifika mwenge waongee kiswahili,kama mambo ndio hayo,au bongo ,zanzibar,na nchi zote zinazo ongea kiswahili,kwanza inabidi tuandamani kwa kuwa huo ni ukoloni wa aina yake unataka kurudi duniani.

    ReplyDelete

Top Post Ad